Smiley face

Jumamosi, 7 Julai 2018

Swahili Worship Song "Unapoufungua Moyo Wako kwa Mungu" | Seeing the Love of God



Wakati hamumwelewi Mungu na hamjui asili Yake,
mioyo yenu haiwezi kamwe kufunguka, kufunguka kwa Mungu.
Mara utakapomwelewa Mungu wako,
utaelewa kile kilicho moyoni Mwake,
na kufurahia kile kilicho ndani Yake
kwa imani na usikivu wako wote.
Unapofurahia kile kilicho ndani ya moyo wa Mungu, kidogo kidogo,
siku baada ya siku,
unapofurahia kile kilicho ndani ya moyo wa Mungu,
moyo wako utakuwa wazi Kwake.
Moyo wako unapokuwa wazi kwa kweli,
moyo wako unapokuwa wazi kwa kweli,
utaona madharau,
utaiona aibu ya maombi yako ya kupita kiasi na yenye ubinafsi.
Moyo wako unapokuwa wazi kwa kweli,
moyo wako unapokuwa wazi kwa kweli,
utaona dunia isiyo na mwisho moyoni mwa Mungu,
na kuwa katika ulimwengu wa maajabu yasiyosimuliwa.
Katika ulimwengu huu hakuna uongo,
hakuna udanganyifu, hakuna giza na hakuna uovu.
Kuna ukweli na uaminifu tu;
haki na ukarimu pekee.
Yeye ni upendo, Yeye anajali,
ana huruma isiyo na mwisho.
Maishani mwako, unahisi furaha,
Unapoufungua moyo wako kwa Mungu.
Hekima na nguvu Zake vinajaza ulimwengu huu,
na vile vile mamlaka na upendo Wake.
Unaweza kuona kile Mungu alicho na Alicho nacho,
kinachomletea furaha,
kinachomletea matatizo, kinachomletea huzuni na hasira,
vyote viko wazi kwa kila mmoja kuona,
unapoufungua moyo wako kwa Mungu
na kumwalika aingie ndani.

kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, ni Bwana Yesu aliyerudi. Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu linajitokeza kwa sababu ya kuonekana kwa kazi ya Mungu na iliyojumuishwa na wale wote waliomkubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya dhati ya siku za mwisho na walishindwa na kuokolewa na neno la Mungu. Kondoo za Mungu husikia sauti ya Mungu. Kwa sababu ya kuonekana kwa maneno ya Kristo wa siku za mwisho, watu zaidi na zaidi ambao wana kiu ya kutafuta ukweli wameshindwa na neno la Mungu na kurudi kwa Mwenyezi Mungu. Wamepata maji ya kunywa na kulishwa na neno la Mungu na kufurahia kazi na mwongozo wa Roho Mtakatifu, wakithibitisha kwa hakika kwamba Mwenyezi Mungu ndiye kurudi kwa Mkombozi ambaye tumemtarajia kwa miaka mingi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni