Smiley face

Jumatano, 6 Desemba 2017

Sura ya 42. Kwa Kutafuta Ukweli tu Ndio Unaweza Kupata Mabadiliko katika Tabia Yako

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa kutafuta ukweli tu ndipo utapata mabadiliko katika tabia yako: Hili ni jambo unalofaa kulielewa na kulielewa vizuri kabisa. Usipoelewa ukweli vya kutosha, utateleza kwa urahisi na kupotoka. Kutafuta kukua katika maisha lazima utafute ukweli katika kila kitu. Haijalishi suala gani laweza kutokea, lazima utafute kukumbana nalo katika njia inayopatana na ukweli, kwa sababu ukikumbana nayo kwa njia isiyo safi kabisa, basi unaenda kinyume na ukweli. Chochote ufanyacho, lazima kila wakati ufikirie thamani yake. Unaweza kufanya yale mambo yaliyo na maana na lazima usifanye mambo yasiyo na maana. Kuhusu mambo ambayo unaweza kuyafanya ama kutoyafanya, kama yanaweza kuachiliwa, basi yaachilie. Ama ukifanya mambo haya kwa muda fulani na lazima uyaachilie, basi yaachilie haraka, ukifanya uamuzi kwa uepesi. Hii ndiyo kanuni unayofaa kufuata unapofanya kitu chochote. Watu wengine wanauliza swali hili: “Mbona ni vigumu sana kutafuta ukweli na kuuweka ukweli katika matendo kugumu vile? Ni kama kuelekeza mashua dhidi ya mkondo; ukiacha kuielekeza mbele basi unarudi nyuma tena. Mbona kufanya mambo maovu ama vitu visivyo na maana sawa na mashua kuufuata mkondo? Kwa kweli inafanyika kwa urahisi sana. Haya yote ni kuhusu nini?” Hii ni kwa sababu asili ya mwanadamu ni ile ya kumsaliti Mungu na kwa sababu ni hali ya kuonyesha hisia ambayo imechukua jukumu la uongozi ndani ya mwanadamu. Asili inayoasi dhidi ya Mungu bila shaka kwa urahisi inaweza kufanya vitu vinavyomsaliti Mungu, na vitu vizuri bila shaka ni vigumu kwake kufanya. Hii inaamuliwa kabisa na ubora wa asili hiyo. Unapoelewa ukweli kwa kweli na unaanza kuupenda ukweli kutoka ndani yako mwenyewe, unakuwa bora kitabia kufanya vitu vinavyopatana na ukweli na unapata nguvu. Inakuwa kawaida, kwa kiwango ambapo unaweza kufanya hivyo kwa njia rahisi na ya furaha, na unahisi kuwa kufanya chochote hasi kinahitaji juhudi kubwa. Hii ni kwa sababu una ukweli na umechukua jukumu la uongozi katika moyo wako. Kama kweli unauelewa ukweli kuhusu maisha ya mwanadamu, kama unaelewa ukweli wa aina gani ya mtu wa kuwa, jinsi ya kuwa mtu wa tabia ya hali ya juu na wazi, mtu mwaminifu, jinsi ya kuwa mtu anayetoa ushuhuda kwa Mungu na kumtumikia Yeye, basi hutafanya tena mambo maovu ambayo yanamkataa Mungu ama kuchukua jukumu la kuwa mpinga Kristo ama chungaji wa uongo. Hata kama mtu angekushawishi, bado hungekifanya; hata angekulazimisha, bado hungetenda kwa njia hiyo. Hii ni kwa sababu una ukweli ndani yako, unaweza kuuchukia uovu, kuhisi chuki ndani kwa vitu hasi, na ingekuwa vigumu kufanya vitu hivi, kwa sababu tabia yako imebadilika. Kama kwa kweli una ukweli ndani mwako, njia unayotembea kiasili itakuwa njia sahihi. Bila ukweli, ni rahisi kufanya uovu na hutaweza kujisaidia mwenyewe. Kwa mfano, kama una kiburi na majivuno ndani mwako, haitawezekana kutomkataa Mungu, lakini badala yake utasababishwa kumkataa. Hutafanya hivyo kimakusudi; utafanya hivyo chini ya utawala wa asili yako ya kiburi na majivuno. Kiburi na majivuno yako vitakufanya umdharau Mungu, vitakufanya umwone Mungu kuwa asiyefaa, vitakufanya ujiinue, vitakufanya kujiweka kila wakati kwenye maonyesho na mwishowe vitakufanya ukae katika nafasi ya Mungu na kujitolea ushuhuda mwenyewe. Mwishowe utatengeneza mawazo yako mwenyewe, fikira zako mwenyewe na dhana zako kuwa ukweli wa kuabudiwa. Tazama ni kiasi gani cha uovu kinafanywa na watu chini ya utawala wa asili yao ya kiburi na majivuno! Kutatua kufanya kwao uovu, mtu anafaa kwanza kutatua tatizo la asili yake. Bila mabadiliko katika tabia, haiwezekani kimsingi kutatua shida hii. Unapokuwa na uelewa fulani wa Mungu, unapoweza kuona upotovu wa mwanadamu na kutambua kiburi na majivuno yanayodharauliwa na mabaya, basi utahisi chuki, kughadhabishwa na kutatizwa. Utaweza kufanya mambo kwa ufahamu kumridhisha Mungu na kwa kufanya hivi utahisi kuridhika. Utaweza kwa ufahamu kutoa ushuhuda kwa Mungu na kwa kufanya hivi utahisi raha. Kwa ufahamu utajifichua mwenyewe na kuweka wazi ubaya wako, na kwa kufanya hivi utahisi vizuri ndani yako na hali yako ya akili itaboreshwa. Kwa hivyo hatua ya kwanza ya kutafuta mabadiliko katika tabia yako ni kutafuta kulielewa neno la Mungu na kuingia katika ukweli. Ni kwa kuuelewa tu ukweli ndio unaweza kuwa na utambuzi; ni kwa kuwa na utambuzi tu ndio unaweza kuelewa mambo kabisa; ni kwa kuelewa mambo tu kwa wazi ndio unaweza kuutelekeza mwili na, hatua kwa hatua, utatembea njia sahihi ya imani kwa Mungu. Hii imeungana na jinsi mwanadamu alivyo na uamuzi anapotafuta ukweli. Kama mtu ana uamuzi wa kweli, baada ya miezi sita ama mwaka mmoja ataanza kuingia katika njia sahihi, ataona matokeo ndani ya miaka mitatu ama mitano, na atahisi kuwa anafanya maendeleo katika maisha. Kama umamwamini Mungu lakini hutafuti ukweli, basi unaweza kuamini kwa miaka 10 na usipate kupitia mabadiliko yoyote, mwishowe ukisema, “Kumwamini Mungu ni hivi, hakuna maana kubwa kwake; ni sawa tu na maisha yangu duniani awali. Hakuna hamu ya kuishi.” Hii inaonyesha kwa kweli kuwa bila ukweli, maisha ni matupu. Unaweza kunena baadhi ya maneno ya kanuni, lakini bado utahisi usiyefarijika na kutokuwa na uhakika. Kama una uelewa fulani kumhusu Mungu, kama unajua jinsi ya kuishi maisha yenye maana, kama unaweza kufanya mambo yanayomridhisha Mungu, basi utahisi kuwa haya ni maisha ya kweli, kuwa kwa kuishi tu kwa njia hii ndiyo maisha yako yatakuwa na maana, kuwa mtu lazima aishi kwa njia hii ili kuweza kumridhisha Mungu kidogo na kuhisi mwenye kuridhika. Kama unaweza kumridhisha Mungu kwa ufahamu, kwa ufahamu kuweka ukweli katika matendo, ujitelekeze mwenyewe kwa ufahamu, uache mawazo yako mwenyewe, na uwe mtiifu na kuyafikira mapenzi ya Mungu; kama unaweza kufanya mambo haya yote kwa ufahamu basi hii ni kuuweka ukweli katika matendo kisahihi, kuuweka ukweli kwa kweli katika matendo na sio kama kutegemea kwako kwa awali kwa mawazo yako na kufuata kwako kanuni na sheria. Kwa ukweli halisi, inachosha sana kufanya chochote unapokosa kuuelewa ukweli, inachosha kufuata kanuni na sheria, inachosha kutokuwa na malengo na kufanya mambo kwa upofu. Ni kwa ukweli tu ndiyo unaweza kuwa huru—huu sio uongo—na kwa ukweli unaweza kufanya mambo kirahisi na kwa njia ya furaha. Watu walio na hali ya aina hii ni wale walio na ukweli, ni wale ambao wamebadilisha tabia zao.
Katika mchakato wa kutafuta kuingia, kila jambo lazima lichunguzwe na kulinganishwa na neno la Mungu na kulinganishwa na ukweli; lazima yafikiriwe kabisa ili kujua jinsi ya kuyafanya kwa njia ambayo inalingana kabisa na mapenzi ya Mungu. Mambo yanayotokea kutoka kwa mapenzi yako kisha yanaweza kuachwa. Utajua jinsi ya kufanya mambo ukizingatia mapenzi ya Mungu na basi utaenda uyafanye, kana kwamba kila kitu kinafuata mkondo wake, na itahisi ikiwa rahisi kabisa. Watu walio na ukweli hufanya mambo kwa njia hii. Kisha unaweza kuonyesha wengine kuwa umebadilisha tabia yako kwa kweli, wengine wataona kuwa kwa kweli una matendo mazuri, na kuwa unafanya mambo kwa njia ya kufuata kanuni, na kufanya kila kitu sawa. Wataona kuwa huyu ni mtu anayeelewa ukweli, ambaye kwa hakika ana mfano fulani wa ubinadamu na, hakika kabisa, neno la Mungu limevuna matokeo nao. Baada ya mtu kuelewa ukweli kabisa, kisha wanaweza kutambua hali zao wenyewe, kuelewa kabisa masuala magumu na kujua jinsi ya kufanya vitu kwa njia sawa. Kama huelewi ukweli, hutaweza kutambua hali zako mwenyewe. Utataka kuasi dhidi yako mwenyewe lakini hutaja jinsi ya kufanya hivyo ama unachoasi dhidi yake; utataka kujiacha mapenzi yako lakini ukifikiria kuwa mapenzi yako yanapatana na ukweli, basi utaweza vipi kuiacha? Pengine unaweza hata kufikiri kuwa imepewa nuru na Roho Mtakatifu na hivyo hutaiacha hata iweje. Kwa hivyo, mtu asipokuwa na ukweli, ni rahisi sana kwake kufikiri kuwa vitu hivyo ambavyo vinatokea kutoka kwa mapenzi yake, na pia uchafu wa mwanadamu, nia nzuri za mwanadamu, mapenzi ya upofu ya mwanadamu na mwenendo wa mwanadamu, vyote ni sawa, kuwa vinazingatia ukweli—basi utaweza vipi kuasi dhidi yao? Kama huelewi ukweli, wala kujua kuuweka ukweli katika matendo ni nini, kama macho yako yamefungwa na hujui ugeukie njia gani kwa hivyo unaweza kufanya mambo tu kulingana na kile unachofikiri ni sawa, basi utafanya mambo mengine ambayo yatapotoka ama makosa, mengine ambayo yatafuata masharti, mengine ambayo yatatokea kwa shauku na kutakuwa na mengine ambayo yatakuwa yametokea kutoka kwa Shetani na kuwa yataleta usumbufu. Watu wasio na ukweli wanafanya mambo kwa njia hii: Kidogo kushoto, kisha kidogo kwa kulia, sahihi dakika moja kisha kupotoka inayofuata, bila usahihi wowote. Wale wasio na ukweli wanaona vitu vibaya, basi watashughulikia masuala vizuri kwa njia gani? Wataweza kutatua vipi shida yoyote? Kulielewa neno la Mungu sio kitu rahisi kufanya, na ukweli ambao watu wanaweza kuelewa pia una kiwango chake. Zaidi ya hayo, watu wanaweza kumwamini Mungu kwa maisha yao yote, ilhali uelewa wao wa neno Lake bado utakuwa kidogo. Hata wale ambao wamepata uzoefu kiasi wanaweza kuepuka kufanya yale mambo ambayo yanamkataa Mungu, kuepuka yale mambo ambayo kwa dhahiri ni maovu, na kuepuka yale mambo ambayo hayamsaidii yeyote. Haiwezekani kwao kufikia hali ambayo haina mchanganyiko wa mapenzi yao wenyewe. Hii ni kwa sababu watu huwaza mawazo ya kawaida, baadhi ya mawazo ya watu yanazingatia neno la Mungu na ni ya kipengele cha uelewa ambacho hakiwezi kuainishwa kama mapenzi ya kibinafsi. Lakini cha msingi ni kutambua mambo ya mapenzi ya kibinafsi ambayo yanaenda kinyume na neno la Mungu, kinyume na ukweli na kinyume na nuru ya Roho Mtakatifu. Kwa hivyo lazima utumie juhudi kwa kuelewa neno la Mungu na ni kwa kuuelewa ukweli tu ndio unaweza kuwa na utambuzi.
Kwa kutafuta kubadilisha tabia yako, lazima ufikie hatua fulani katika uelewa wako mwenyewe ambayo unaweza kugundua sumu iliyopo katika asili yako mwenyewe. Lazima ujue kumpinga Mungu ni nini na kumuasi Mungu ni nini, na kujua jinsi ya kufanya mambo kulingana na ukweli katika kila suala. Lazima pia uelewe kiasi fulani cha mapenzi ya Mungu na mahitaji Yake kwa mwanadamu. Lazima uwe na dhamiri na busara mbele ya Mungu, na usijivune ama kumdanganya Mungu. Hili linafikia mabadiliko katika tabia yako. Wale ambao wamebadilisha tabia zao wana moyo wa kumwogopa Mungu. Kuna uwezekano mdogo kwa wao kuasi dhidi ya Mungu na wanafanya mambo machache ambayo yanamkataa Mungu. Katika kufanya kazi zao Mungu hahitaji kuwa na wasiwasi kila wakati kuwahusu na Roho Mtakatifu hahitaji kila wakati kufanya kazi ya nidhamu kwao. Kimsingi wanaweza kumtii Mungu na ukweli upo katika mitazamo yao juu ya vitu—hii inafikia kulingana na Mungu. Tuseme mtu akupe kazi fulani, kazi ambayo haihitaji mtu yeyote kukusimamia. Unakamilisha tu kazi hii kulingana na neno la Mungu na kupitia maombi na, katika kazi hii, una uwezo wa kutokuwa na kiburi na majivuno, kutofanya chochote ambacho kinamkataa Mungu, kutomzuia mwingine yeyote na unaweza kuwasaidia wengine kwa huruma. Kwa subira unaweza kupitisha uzoefu wako katika ushirika kwa wengine ili kila mmoja apate ukimu, wapate faida, na kuweza kuingia katika njia sawa ya kumwamini Mungu. Zaidi, katika kazi hii hautafuti hadhi yako mwenyewe ama maslahi, usichukue chochote ambacho haukuchuma mwenyewe, usinene kwa ajili yako mwenyewe, na bila kujali vyovyote unavyotendewa na mwingine, watendee wote vizuri. Basi hapo utakuwa mtu mwenye kimo kizuri. Sio jambo rahisi kwa mtu kuchukua kazi na kumleta kila mtu katika ukweli wa neno la Mungu. Kuna wengi ambao wana vipaji vikubwa ambao wanaanguka na kuvunjika. Bila ukweli watu hawawezi kutegemewa kabisa, hata kwa uchache zaidi kama hawajabadili tabia zao. Kimo chako ni gani sasa? Unafaa kumtendea vipi mtu anayekusifu? Unafaa kutendea vipi mtu aliye na maoni kukuhusu, ama anakuangalia kwa kukosoa? Je, unaweza kukuza na kuchagua watu sawa bila kutegemea hisia zako mwenyewe? Je, mnaweza kweli kufanya mambo haya na kimo chenu kilivyo sasa? Kama watu wengi wanaona ufanyacho kikiwa kizuri na kinafaa, basi hiyo ni sawa, na unafaa kutumiwa. Kama ulifanya kazi mahali fulani kwa miaka kadhaa na watu wengi walifikiria vibaya kukuhusu, basi hii inaonyesha kuwa hujahitimu na hufai kwa Mungu kukutumia. Haiwezekani kufikia hatua ambapo unafaa kutumiwa na Mungu kama huna ukweli.
Katika kutafuta maisha, lazima utilie maanani vitu viwili vya msingi: 1) kuelewa ukweli ndani ya neno la Mungu, na 2) kujielewa mwenyewe ndani ya neno la Mungu. Vitu hivi viwili ni muhimu sana. Hakuna maisha ama ukweli nje ya neno la Mungu. Usipotafuta ukweli ndani ya neno la Mungu, basi ni wapi kwingine utatafuta? Ni wapi kuna ukweli duniani? Je, vitabu vyote vilivyochapishwa duniani sio nadharia ya ibilisi Shetani? Je, ukweli wowote wa kuzungumziwa upo wapi? Kitu cha maana zaidi katika kuelewa ukweli katika neno la Mungu ni pamoja na kumwelewa Mungu katika neno Lake, uelewa wa maisha ya mwanadamu katika neno Lake na uelewa wa vipengele vyote vya ukweli katika neno Lake. Kwa mfano, uelewa wa kweli wa mtu mwenyewe na kugundua maana ya uwepo wa mwanadamu katika neno la Mungu.... Ukweli wote uko katika neno la Mungu. Huwezi kuingia katika ukweli isipokuwa ifanyike kupitia katika neno la Mungu. Tokeo kuu ambalo lazima ufikie ni kujua uelewa wa kweli wa neno la Mungu ni nini. Na uelewa wa kweli wa neno la Mungu unaweza basi kuuelewa ukweli: Hiki ni kitu cha maana sana. Watu wengine wanafanya kazi na kuhubiri ibada na, ingawa kwa juu inaonekana kana kwamba wanashiriki kuhusu neno la Mungu, wanachosema ni maana halisi ya neno la Mungu, na asili ya neno ikiachwa kabisa bila kunenwa. Ibada zao ni kama kufunza kutoka kwa kitabu cha lugha, kikiwa kimepangwa kipengee kwa kipengee, kipengele kwa kipengele, na wanapomaliza kila mmoja anaimba sifa zao, wakisema: “Ah, mhubiri huyu ni mtu wa vitendo sana. Alihubiri vizuri sana na kwa maelezo ya kina.” Baada ya kumaliza kuhubiri, anawaambia wengine waweke pamoja kile ambacho kimehubiriwa na kumpa kila mtu. Kwa kufanya hivi, anawadanganya wengine na kile anachohubiri ni uongo. Kwa juu, inaonekana kana kwamba anahubiri tu neno la Mungu na kuwa maneno yake yanazingatia ukweli. Lakini ukitambua kwa makini, utaona kuwa yote asemayo ni maneno ya mafundisho na ni hoja za uongo. Maneno yake pia yana ubunifu fulani, dhana na kuna maneno ambayo yanamueleza Mungu. Je, kuhubiri kwa namna hii hakudakizi kazi ya Mungu? Ni njia ya kuhudumu inayomkataa Mungu. Mtu mwenye busara lazima aweke mipaka katika mawanda ya hotuba yake mwenyewe—ni vipengele gani vya hotuba wanafaa kusema na gani vinahusiana na wajibu wao, na vipengele gani vya hotuba vinaweza kunenwa tu na Mungu. Mwanadamu hapaswi kusimama na kunena katika nafasi ya Mungu. Jinsi Mungu anavyofanya kazi, hakuna anayeweza kuelewa, kwa hivyo mtu yeyote anaweza vipi kumfafanua Mungu? Mwanadamu hajahitimu hata kidogo kumfafanua Mungu na hili lazima lieleweke ili kuepuka kufanya chochote kisicho cha busara. Kama mtu mwenye busara, lazima ujue nafasi yako, ujue mambo sawa ya kusema na, ingawa unaweza kuwa umekuja kujua jambo, unajua kutosema chochote ambacho hufai kusema. Hata kama Mungu alikuambia jambo awali, hufai kulirudia kwa wengine; kutakuwa na faida gani kulisema? Je, haitakuwa kiburi kutaka kila wakati kuwa juu ya kituo chako kwa kuongea tu? Kama huelewi masuala ya Mungu basi huyaelewi. Usijifanye kuelewa ama kuwa mjua yote. Haivutii! Kila wakati unataka kusimama mahali pa Mungu ili kuonyesha kuwa unaelewa kila kitu na kujichukulia sifa. Pia unataka kunena mengi na kumfanyia Mungu mengi. Kila mtu ana tamaa hii na ni kitu cha aibu sana. Sasa wageni wanakuja kutafuta njia ya kweli, kwa hivyo unafaa vipi kutoa ushuhuda kwa Mungu? Kama huna busara, una kiburi na majivuno na unafanya mambo kwa upofu, je, basi haumkatai Mungu na kumkufuru Yeye? Je, hii ni kufanya wajibu wako? Hata kwa uchache, huku ni kutoa ushahidi kwa Mungu. Hii kwa kweli ni wewe kufichua sura yako ya Shetani. Wale ambao kwa kweli wameshidnwa lazima wajifunze jinsi ya kunena kwa dhati na kutoa ushuhuda wa kweli. Kusshiriki uzoefu wa maisha yako na wengine ni bora kuliko chochote kingine. Kujivuna na kuongea juu ya nadharia kuu—hii ina faida gani? Baada ya kupata uzoefu wa kazi ya Mungu kwa miaka mingi, bado tabia ya mwanadamu sio nzuri, na mwanadamu hafai kutoa ushuhuda kwa Mungu, kulingana na utambulisho wao. Bila busara na kiburi, mwanadamu bado anataka kutoa ushuhuda kwa Mungu. Je kwa kweli humwaibishi na kumkufuru Mungu? Humwelewi Mungu. Zaidi ya hayo, tabia yako bado inamkataa Mungu. Kwa hivyo hakuna hata harufu ya chukizo juu yako kutoa ushuhuda? Je hakuna kitu cha kukirihi kuihusu? Kwa hivyo mwandamu hafai kutoa ushuhuda kwa Mungu. Mtu akisema: “Unaweza kutushuhudia kazi ya Mungu katika Uchina bara?” unasema: “Nimepata uzoefu wa kazi ya Mungu wa miaka kadhaa, kwa hivyo nafikiri tumehitimu kutoa ushuhuda kwa Mungu.” Je, hili sio tatizo? Kwa mara nyingine hii sio busara! Mwanadamu hafai kutoa ushuhuda kwa Mungu. Unafaa tu kusema: “Hatufai kutoa ushuhuda kwa Mungu. Ilhali Mungu ametuokoa na kutupa neema. Tumepata neema kidogo na tumepata uzoefu kidogo wa neno la Mungu, kwa hivyo tunaweza kushiriki katika ushirika, lakini hatuwezi kufikiria kutoa ushuhuda kwa Mungu. Tukizungumza kuhusu kutoa ushuhuda kwa Mungu, hatujahitimu; tunaweza tu kuongelea uzoefu wetu wenyewe.” Ni sawa kwako kushiriki jinsi wewe mwenyewe umepata uzoefu wa kutwaliwa na Mungu, ulivyokuwa umepotoka katika wakati huo, ulivyokuwa na kiburi, aina gani ya tokeo ulipata mwishowe baada ya kutwaliwa, na aina gani ya azimio ulikuwa nalo mwishowe. Kwa kweli, hii ndiyo njia ya kutoa ushuhuda ambayo Mungu anamhitaji mwanadamu kufuata, na njia hii inapatana kabisa na mapenzi ya Mungu. Ukisema unataka kutoa ushuhuda kwa Mungu na unataka kuchukua nafasi ambapo unaweza kutoa ushuhuda kwa Mungu, basi hili ni kosa kubwa—huna busara na una kiburi. Unaweza tu kusema: “Tunaweza kuongelea uzoefu fulani lakini hatuwezi kufikiria kutoa ushuhuda kwa Mungu. Nitashiriki kitu kwanza. Kwa nini Mungu alipata mwili katika Uchina? Labda hamwelewi vizuri. Tumeelewa hili kutoka kwa kazi ya Mungu. Sisi Wachina tumepotoshwa zaidi na Shetani, na tuko katika mahali ambapo joka kubwa jekundu limelala likiwa limejikunja. Tumepotoshwa sana na Shetani, ubinadamu wetu umepungukiwa sana, tuna uadilifu wa chini sana na hatukai kama binadamu hata kidogo. Ikilinganishwa na watu waliochaguliwa wa Mungu kutoka mataifa yote mengine na kanda zote, sisi ndio duni kabisa. Kwa hivyo tuna aibu sana kutoa ushuhuda kwa Mungu. Tunaweza tu kutoa ushuhuda kidogo kwa uzoefu wetu wenyewe. Sisi ni watu wachafu sana na waliopotoka sana, na tumeletwa ndani ya wokovu mkubwa wa Mungu na tumepata upendo mkuu wa Mungu, kwa hivyo lazima tunene kuhusu ushuhuda wa uzoefu wetu wa kibinafsi, na hatuwezi kuizuia neema ya Mungu.”
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Kujua zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni