Smiley face

Jumatatu, 10 Juni 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III
Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii: Awamu Sita katika Maisha ya Binadamu Kuzaliwa: Awamu ya Kwanza 1. Maisha Mapya Yanazaliwa Kulingana na Mipango ya Muumba 2. Kwa Nini Binadamu Tofauti Wanazaliwa Katika Hali Tofauti Kukua: Awamu ya Pili 1. Hali Ambazo Mtu Hukulia Ndani Zimepangwa na Muumba 2. Hali Mbalimbali Ambazo Watu Hukulia Ndani Husababisha Wajibu Tofauti
   
          Mwenyezi Mungu anasema:

Hakuna yeyote aliye na chaguo kuhusu sehemu hizi za awamu hii; zote ziliamuliwa kabla, mapema kabisa na Muumba. Haziathiriwi na mazingira ya nje kwa vyovyote vile, na hakuna masuala yanayosababishwa na binadamu yanaweza kubadilisha hoja hizi ambazo Muumba aliamua kabla. Kwa mtu kuweza kuzaliwa inamaanisha kwamba Muumba tayari ametimiza hatua ya kwanza ya hatima ambayo Amempangilia mtu huyo. Kwa sababu Aliamua kabla maelezo haya yote tena mapema mno, hakuna aliye na nguvu za kubadilisha maelezo yoyote yale. Licha ya hatima ya baadaye ya mtu, hali za kuzaliwa kwa mtu ziliamuliwa kabla, na zinabakia kama zilivyo; haziathiriwi kwa njia yoyote ile na hatima ya mtu katika maisha, wala haziathiri kwa vyovyote vile ukuu wa Muumba juu yazo.
Tazama Video: Matamshi ya Mungu | "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II) Sehemu ya Kwanza" Yaliyopendekezwa: Sauti ya Mungu




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni