Smiley face

Jumatatu, 11 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | “Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu”


Matamshi ya Mungu | “Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu”


Mwenyezi Mungu anasema, “Katika maisha yenu ya kila siku, mnaishi katika hali na mazingira yasiyo na ukweli ama fahamu nzuri. Hamna rasilimali ya uwepo na pia hamna msingi wa Kunijua au kujua ukweli. Imani yenu imejengwa tu juu ya ujasiri usio dhahiri au kwenye ibada za kidini na ujuzi kulingana na mafundisho ya kidini kabisa.
Kila siku Ninatazama mienendo yenu na kuchunguza nia yenu na matunda yenu maovu. Sijawahi kumpata mmoja ambaye kwa kweli aliweka moyo wake na roho yake kwenye madhabahu Yangu, ambayo hayajawahi kusonga. Kwa hivyo, Singependa kuyamwaga bure maneno yote ambayo Nina nia ya kumwelezea mwanadamu wa aina hii. Moyoni Mwangu, Ninapanga kuikamilisha kazi Yangu iliyosalia tu na kuleta wokovu kwa mwanadamu ambaye Sijamwokoa bado. Hata hivyo, Ningependa wale wote wanaonifuata wapokee wokovu Wangu na ukweli ambao neno Langu linaweka katika mwanadamu. Natumaini kuwa siku moja unapofumba macho yako, utauona ulimwengu ambamo manukato yametanda hewani na vijito vya maji ya uhai vinatiririka, na wala sio dunia baridi isiyoonekana vizuri ambapo giza limetanda angani na ambamo vilio vya kughadhabisha havikomi.”

kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni