Smiley face

Alhamisi, 13 Juni 2019

Maonyesho ya Mungu | "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu" Sehemu ya Tano



Maonyesho ya Mungu | "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu" Sehemu ya Tano

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu "Neno Laonekana katika Mwili".
Maudhui ya video hii: Aina Tano za Watu Aina ya Kwanza: Hatua ya Mtoto Mchanga aliyefungwa kwa Vitambaa Aina ya Pili: Hatua ya Mtoto Mchanga Anayenyonya Aina ya Tatu: Hatua ya Mtoto Mchanga Anayeachishwa Ziwa, au Hatua ya Mtoto Mdogo Aina ya Nne: Hatua ya Mtoto Anayekomaa, au Kipindi cha Utoto Aina ya Tano: Hatua ya Maisha Yaliyokomaa, au Hatua ya Mtu Mzima
Mwenyezi Mungu anasema:
Kwa sasa, Nitaacha ushirika wetu kuhusu tabia ya haki ya Mungu umalizikie hapo. Kinachofuata Nitaainisha wafuasi wa Mungu katika kategoria mbalimbali, kulingana na ufahamu wao wa Mungu na ufahamu wao na kile wamepitia kuhusiana na tabia ya haki Yake, ili muweze kujua awamu ambayo kwa sasa mnapatikana ndani pamoja na kimo chenu cha sasa. Kuhusiana na maarifa yao ya Mungu na ufahamu wao wa tabia Yake ya haki, awamu na kimo tofauti ambavyo watu huwa navyo vinaweza kugawanywa katika aina tano. Mada hii imeelezewa kwa msingi wa kumjua Mungu wa kipekee na tabia Yake ya haki; kwa hivyo, unaposoma maudhui yafuatayo, unafaa kujaribu kwa makini kuchambua ni kiwango kipi haswa cha ufahamu na maarifa ulichonacho kuhusiana na upekee wa Mungu na tabia Yake ya haki, na kisha utumie hayo kujua ni awamu gani ambayo kwa kweli unapatikana ndani, kimo chako ni kikubwa vipi kwa kweli, na wewe ni aina gani ya mtu kwa kweli. Tazama Video: Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu" Yaliyopendekezwa: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni