Smiley face

Alhamisi, 31 Oktoba 2019

Ninapata njia ya kumjua Mungu

Ninaona njia ya kumjua Mungu
Xiaocao Mji wa Changzhi, Mkoa wa Shanxi
Siku moja, niliona kifungu hiki kifuatacho cha neno la Mungu kwa maandishi “Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu”: “Katika kipindi kile alichomfuata Yesu, Petro alitazama na kutia moyoni kila kitu kuhusu maisha Yake: Matendo Yake, maneno Yake, mwendo Wake na maonyesho Yake. … Tangu wakati huo akiwa na Yesu, Petro alitambua pia kwamba hulka Yake ilikuwa tofauti na ile ya binadamu wa kawaida. Siku zote alikuwa na mwenendo dhabiti na hakuwahi kuwa na haraka, hakupigia chuku wala kupuuza chochote, na aliyaishi maisha Yake kwa njia iliyokuwa ya kawaida na ya kuvutia. Katika mazungumzo, Yesu alikuwa mwenye madaha na uzuri, mwenye uwazi na mchangamfu ilhali pia mtulivu, na Hakuwahi kupoteza heshima Yake katika utekelezaji wa kazi Yake. Petro aliona kwamba Yesu wakati mwingine alikuwa mnyamavu, ilhali nyakati nyingine alizungumza kwa mfululizo. Wakati mwingine Alikuwa na furaha sana kiasi cha kwamba aligeuka na kuwa mwepesi na mchangamfu kama njiwa, na ilhali nyakati nyingine Alihuzunika sana kiasi cha kwamba hakuzungumza kamwe, ni kana kwamba alikuwa mama aliyeathirika na hali ya hewa. Nyakati nyingine Alijawa na hasira, kama askari jasiri anayefyatuka kuwaua adui, na wakati mwingine hata kama simba anayenguruma. Nyakati nyingine Alicheka; nyakati nyingine aliomba na kulia. Haijalishi ni vipi Yesu alivyotenda, Petro alizidi kuwa na upendo na heshima isiyokuwa na mipaka Kwake. Kicheko cha Yesu kilimjaza kwa furaha, huzuni Yake ikamtia simanzi, hasira Yake ikamtetemesha, huku huruma Zake, msamaha na ukali vyote vikamfanya kuja kumpenda Yesu kwa kweli, na akaweza kumcha na kumtamani kwa kweli. Bila shaka, Petro alikuja kutambua haya yote kwa utaratibu baada ya kuishi kando yake Yesu kwa miaka michache” (Neno Laonekana katika Mwili).

Jumatano, 30 Oktoba 2019

Maneno ya Mungu Yaliondoa Dhana Zangu

Maneno ya Mungu Yaliniongoza Kutoka Katika Matatizo
Xiao Rui Mji wa Panzhihua, Mkoa wa Sichuan
Nilipokuwa nikihubiri injili nilikutana na viongozi wa dini ambao walisema uongo ili kupinga na kuvuruga, na kuwaita polisi. Hili lilisababisha wale niliokuwa nikihubiria kutothubutu kuwasiliana nasi, na wale ambao walikuwa tu wameikubali injili kutoweza kuwa na imani katika kazi ya Mungu. Nilipofanya kazi kwa bidii sana lakini matokeo yalikuwa duni, nilifikiri: kazi ya Kiinjili ni ngumu sana kutekeleza. Lingekuwa jambo la kustaajabisha sana kama Mungu angeonyesha miujiza kiasi na kuwaadhibu wale ambao husema uongo pamoja na wale ambao kwa uzito kabisa humpinga Mungu kuwaonyesha wale ambao wamedanganywa. Basi si kazi ya injili ingetekelezwa kwa haraka zaidi? Haingekuwa vigumu sana kwetu kuhubiri injili.... 

Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu

Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu
Qingxin Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan
Zamani, sikuelewa kazi ya Mungu ya kuwaokoa binadamu. Nilidhani kuwa almradi mtu fulani hufichua upotovu katika kazi yake au hufanya makosa ambayo huiharibu kazi ya kanisa, mtu huyo atakabiliwa na rada, au kupoteza kazi yake au aathiriwe na adhabu. Hiyo ni haki ya Mungu. Kutokana na ufahamu huu usio sahihi, pamoja na hofu ya kupoteza kazi yangu kutokana na kufanya makosa katika kazi yangu, nilifikiria juu ya utaratibu “mjanja”: Wakati wowote ninapofanya kitu vibaya, mimi hujaribu niwezavyo kutowaacha viongozi wajue kwanza, na kwa haraka kujaribu kukifidia mwenyewe na kufanya kila linalowezekana ili kukisawazisha. Je, si hilo basi litanisaidia kuhifadhi kazi yangu? Kwa hiyo, wakati wowote nilipowapa ripoti juu ya kazi yangu, ningepunguza masuala makubwa kuwa madogo na masuala madogo kuwa si kitu. Iwapo wakati mwingine nilikuwa baridi ningefanya liwezekanalo ili kulifunika mbele ya viongozi na kujifanya kuwa mtendaji zaidi na chanya, nikiwa na hofu kwamba viongozi wangenifikiria kuwa asiyeweza na kuacha kunitumia. Hiyo hivyo tu, ningelindwa kwa makini sana dhidi ya Mungu na viongozi katika kila kitu nilichokifanya.

Jumatatu, 28 Oktoba 2019

Mimi Sistahili Kumwona Kristo

Mimi Sistahili Kumwona Kristo
Huanbao Mji wa Dalian, Mkoa wa Liaoning
Tangu kwanza nianze kumwamini Mwenyezi Mungu, daima nimewapenda wale ndugu wa kiume na wa kike ambao wanaweza kupokea huduma ya kibinafsi ya Kristo, ambao wanaweza kusikia mahubiri Yake kwa masikio yao wenyewe. Katika moyo wangu, nimewaza jinsi ingekuwa vizuri sana kama siku moja katika siku zijazo ninaweza kusikia mahubiri ya Kristo, bila shaka kumwona Yeye kungekuwa kwa ajabu hata zaidi. Lakini hivi karibuni, kwa njia ya kusikiliza ushirika Wake, nimekuja kuhisi kwa undani moyoni mwangu kwamba mimi sifai kumwona Kristo.

Jumapili, 27 Oktoba 2019

Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake

Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake
Hu Ke Mji wa Dezhou, Mkoa wa Shandong
Wakati wowote nilipoona maneno haya yaliyosemwa na Mungu, nilihisi kuwa na wasiwasi: “Kila sentensi Niliyoizungumza ina tabia ya Mungu ndani yake. Mngefanya vizuri endapo mngetafakari kuhusu maneno Yangu kwa umakini, na kwa kweli mtafaidi pakubwa kutoka kwa maneno hayo” (“Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Nilihisi kuwa na wasiwasi kwa sababu kuelewa tabia ya Mungu ni muhimu sana yote kwa ufahamu wa mwanadamu wa Mungu na kutafuta kumpenda na kumridhisha Yeye. Lakini wakati wa kula na kunywa maneno ya Mungu, siku zote nilihisi kama tabia ya Mungu ilikuwa dhahania mno, na sikujua jinsi ya kuielewa. Baadaye, kupitia kwa ushirika kutoka kwa kiongozi wangu, nilikuja kujua kwamba ni lazima nielewe kile ambacho Mungu anapenda na kile Anachokichukia kutoka kwa maneno Yake, na hivyo kuelewa tabia ya Mungu. Baadaye nilijaribu kwa muda kuweka jambo hili katika matendo na niliona matokeo. Lakini bado nilihisi kuchanganyikiwa kuhusu maneno ya Mungu, “Kila sentensi Niliyoizungumza ina tabia ya Mungu ndani yake,” na sikuwa na wazo la jinsi ya kuyaelewa hasa.

Jumamosi, 26 Oktoba 2019

Baada ya Kupoteza Hadhi Yangu …

Umwombe Mungu
Huimin Mji wa Jiaozuo, Mkoa wa Henan
Kila wakati nilipoona au kusikia kuhusu mtu aliyekuwa amebadilishwa kama kiongozi naye kujisikia mwenye huzuni, dhaifu au mnunaji, basi niliwaangalia kwa dharau. Nilidhani haikuwa kitu zaidi ya watu tofauti waliokuwa na majukumu tofauti ndani ya kanisa, kwamba hakukuwa na tofauti kati ya juu au chini, kwamba sote tulikuwa uumbaji wa Mungu na hakukuwa na sababu ya kuhuzunikia. Kwa hiyo kama nilikuwa nikiwatunza waumini wapya au kuongoza wilaya, sikuwahi kufikiri kuwa nilizingatia sana hadhi yangu, kwamba nilikuwa mtu wa aina hiyo. Singeweza kamwe kufikiri hata katika miaka milioni moja kwamba ningeonyesha tabia ya aibu kama hiyo wakati mimi mwenyewe nilipobadilishwa …Kwa kuwa kazi yangu haikuwa imeleta matokeo yoyote kwa muda fulani, kiongozi wangu alinibadilisha. Wakati huo, nilidhani kuwa hata kama ubora wa tabia yangu haukuwa umefanywa kuwa kiongozi wa wilaya, hakika ni lazima bado niruhusiwe kufanya kazi ya kunyunyizia. Sikuwahi kutarajia kiongozi wangu anifanye nitunze kazi za kawaida. Nilishangaa basi, nikifikiria kuwa kiongozi wa wilaya mwenye heshima kama mimi leo akitumwa, na kwamba mtu yeyote katika kanisa ambaye angeweza kupeleka ujumbe au ambaye alikuwa na akili kidogo angeweza kufanya kazi hii. Je, si kunilazimisha nifanye kazi hii ulikuwa dhahiri ni uharibifu wa vipaji vyangu? Lakini niliendelea kujiwekea hisia zangu, nikiwa na hofu kwamba dada zangu wangesema sikuwa mtiifu, kwamba nilijali kuhusu hadhi yangu. Lakini mara tu nilipofika nyumbani, nilianguka sawasawa kitandani na kujisikia vibaya sana. Mawazo ya kutokuwa na hadhi kutoka sasa kwendelea na kushangaa ni jinsi gani ndugu zangu wa kike na wa kiume wangeniona yalijaa kichwani mwangu. Na kunifanya nitumwe—ningewezaje kupata umaarufu wangu tena? Nilivyozidi kulifikiria jambo hilo, ndivyo nilivyozidi kujihisi vibaya sana.

Ijumaa, 25 Oktoba 2019

Kuona Uhalisi Wangu Kwa Dhahiri

Mahusiano ya binadamu,Mtu mwaminifu
Xiaoxiao Jijini Xuzhou, Mkoani Jiangsu
Kwa sababu ya mahitaji ya kazi ya kanisa, nilihamishwa mpaka mahali pengine ili kutimiza wajibu wangu. Wakati huo, kazi ya injili mahali pale ilikuwa katika hali duni, na hali ya akina kaka na dada kwa kawaida haikuwa nzuri. Lakini kwa kuwa nilikuwa nimeguswa na Roho Mtakatifu, bado nilijitwisha kila kitu nilichoaminiwa nacho kwa matumaini kamili. Baada ya kukubali kuaminiwa, nilihisi uwajibikaji kamili, kupata nuru kamili, na hata nikafikiri kwamba nilikuwa na uamuzi kiasi fulani. Niliamini kuwa nilikuwa na uwezo na ningeweza kutekeleza kazi hii vizuri. Kwa kweli, wakati huo sikuwa na maarifa kabisa ya kazi ya Roho Mtakatifu au ya asili yangu mwenyewe. Nilikuwa naishi kabisa katika kujiridhisha na kujitamani.

Alhamisi, 24 Oktoba 2019

Kanuni Zangu za Maisha Ziliniacha Nikiwa Nimeharibika

Kanuni Zangu za Maisha Ziliniacha Nikiwa Nimeharibika
Changkai Mji wa Benxi, mkoa wa Liaoning
Maneno ya kawaida “Wote huwekelea mizigo kwa farasi anayekubali” ni ambayo mimi binafsi ninayafahamu sana. Mimi na mume wangu sote tulikuwa hasa watu wasio na hatia: Wakati wa masuala yaliyohusisha faida au hasara yetu binafsi, hatukuwa aina ya watu wa kubishana na kusumbuana na wengine. Pale ambapo tuliweza kuwa wavumilivu tulikuwa wavumilivu, pale ambapo tungeweza kuwa na fadhila tulifanya tulivyoweza kuwa na fadhila. Kama matokeo yake, mara nyingi tulijipata tukiwa tumedanganywa na kudhulumiwa na wengine. Kwa hakika ilionekana kuwa katika maisha, “Wote huwekelea mizigo kwa farasi anayekubali”—iwapo una huruma nyingi sana katika moyo wako, iwapo una fadhila nyingi sana na mwenye staha katika mambo yako, uko katika hatari kuu ya kudanganywa. Nikiwa na mawazo haya katika akili yangu, niliamua kutojiingiza katika unyanyasaji huu wote na kuishi katika matatizo tena: Katika masuala ya siku zijazo na katika kujishughulisha na watu wengine, ninaapa ya kwamba sitakuwa mwenye fadhila nyingi. Hata baada ya kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu, bado nilitumia kanuni hii katika kuendesha tabia yangu na kutangamana kwangu na wengine.

Jumatano, 23 Oktoba 2019

Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo

Mafarisayo
Suxing Mkoa wa Shanxi
Mimi ni mtu mwenye kiburi na majivuno, na cheo kimekuwa udhaifu wangu. Kwa miaka mingi katika imani yangu, nimefungwa na sifa na cheo na sijaweza kujiweka huru kutoka kwazo. Mara kwa mara nimepandishwa cheo na kubadilishwa na mtu mwingine; nimekuwa na vizuizi vingi katika cheo changu na nimekumbwa na matuta mengi njiani. Baada ya miaka mingi ya kushughulikiwa na kusafishwa, nilihisi kwamba sikuwa nachukulia cheo changu kwa uzito. Sikutaka kuwa kama nilivyokuwa katika nyakati zilizopita nikifikiri kwamba mradi nilikuwa kiongozi ningeweza kukamilishwa na Mungu na kwamba iwapo sikuwa kiongozi, basi sikuwa na matumaini. Nilielewa kwamba pasipo kujali jukumu ambalo nilikuwa natimiza, nilihitaji tu kutafuta ukweli na ningefanywa kamili na Mungu; kufuatilia sifa na cheo ni njia ya yule anayempinga Kristo. Sasa ninahisi kwamba pasipo kujali jukumu ambalo ninatimiza, naweza kubali kutokuwa na cheo. Ni sheria ya mbingu na dunia kwamba uumbaji utimize wajibu wake. Haijalishi pale unapowekwa, unapaswa kukubali mipango ya Mungu. Wakati upotovu wa umaarufu na cheo unafichuliwa, unaweza kutatuliwa kwa kuutafuta ukweli. Haijalishi ninachokabiliwa nacho wakati ninatimiza wajibu wangu, mradi ninauelewa ukweli nitakuwa tayari kulipia gharama. Kwa kuzingatia haya, nilifikiri kuwa nilikuwa tayari nimetembea njia ya kutafuta ukweli. Nilifikiri kwamba nimepata tena utu na mantiki. Mungu hupekua moyo na kuchunguza akili. Alijua kwamba nilikuwa mwenye najisi katika kutafuta kwangu ukweli, na kwamba sikuwa kweli natembea njia ya kuutafuta ukweli. Mungu alijua mbinu ya kutumia ili kunitakasa na kuniokoa.

Jumanne, 22 Oktoba 2019

Kuna Njia ya Kumaliza Kiburi

Mahusiano ya binadamu
Xiaochen Jijini Zhengzhou, Mkoani Henan
Kiburi ni dosari yangu ya mauti. Nilikuwa mara kwa mara nikifichua tabia yangu ya kiburi, kila mara nikifikiri kuwa nilikuwa bora kuliko watu wengine. Hasa niliporekebisha ibara au kuwasiliana kuhusu kazi na mbia, kila mara nilikuwa mshupavu na sikusikiliza maoni mengine kwa ustaha. Kutoweza kwangu kushirikiana kwa upatano na wabia wangu mara nyingi kulisababisha matatizo kwa kazi. Ndugu walileta suala hili mara nyingi kwangu, na pia nilisoma mara kwa mara kuhusu Mungu akifichua asili ya watu yenye kiburi. Lakini kwa sababu sikuwa nimepata ufahamu wa kweli wa asili yangu na hali na pia singeweza kuuchukia kweli, wakati wowote nilipokutana na mazingira ya kufaa ningepoteza udhibiti. Baadaye, pia ningehisi kuchukizwa sana, lakini kwa sababu lile lilichofanyika limefanyika, yote niliyoweza kufanya ni kuzidi kujaribu kulielewa. Na hivyo lilifanyika tena na tena. Hilo lilinifanya nihisi aibu sana na nisiyejiweza.

Jumatatu, 21 Oktoba 2019

Ni Nini Husababisha Uongo

Xiaojing Jijini Heze, Mkoani Shandong
Kila mara nilipoona neno la Mungu likituomba kuwa watu waaminifu na kuzungumza kwa usahihi, niliwaza, “Sina tatizo na kuzungumza kwa usahihi. Si ni kusema tu kitu jinsi kilivyo na kusema mambo jinsi yalivyo? Je, hiyo si rahisi? Kilichokuwa kimenikera zaidi daima katika dunia hii walikuwa watu waliotia chumvi walipozungumza.” Kwa sababu ya hili, nilihisi imani kuu, nikifikiri kwamba sikuwa na shida katika hali hii. Lakini kupitia tu kwa ufunuo wa Mungu ndio niligundua kwamba, bila kuingia katika ukweli au kubadili tabia ya mtu, mtu hawezi kwa vyovyote kuzungumza kwa usahihi.Wakati mmoja, niliona kwamba XX hakuwa na utunzaji na kujali kuelekea kwa hali ya kimwili ya wengine, kwa hivyo nilisema kwamba hakuwa na huruma. Baadaye, ni kupitia tu katika ushirika ndiyo nilielewa kwamba upendo wetu wa kweli kwa kila mmoja unajumuishwa kimsingi katika ushirikiano wa pamoja na usaidizi tunaoleta katika kuingia kwetu katika maisha. Wakati mwingine, nilipoona XX akitumia zaidi dola kadhaa wakati wa wajibu wake, nilisema kwamba mtu huyu alikuwa na asili ambayo ni yenye uroho sana. Ni baadaye tu ndiyo niligundua kwamba kuna tofauti kati ya watu wanaoonyesha tabia ya upotovu kidogo na kuwa na asili ya aina hiyo. Kisha kulikuwa na wakati mwingine ambapo kiongozi wangu aliniuliza kuhusu hali ya dada fulani. Kwa sababu nilikuwa na mawazo ya awali kumhusu dada huyu, hata ingawa nilijua wakati huo kwamba nilipaswa kutoa ripoti isiyoegemea upande wowote, bado sikuwa na budi bali kusema kwa ukali kuhusu upotovu ambao alikuwa amedhihirisha, na kukosa kusema hata neno moja kuhusu sifa zake nzuri. Wakati kulitokea mkengeuko au dosari katika kazi yangu mwenyewe, kila wakati ningeripoti hali hiyo kwa viongozi kisirisiri, nikificha ukweli wa mambo ya hakika ili kulinda sura na hadhi yangu. …

Jumapili, 20 Oktoba 2019

Mwanadamu Anaweza Kuokolewa Katikati ya Usimamizi wa Mungu Pekee

Mwanadamu Anaweza Kuokolewa Katikati ya Usimamizi wa Mungu Pekee

Mwanadamu Anaweza Kuokolewa Katikati ya Usimamizi wa Mungu Pekee

Kila mtu anahisi kuwa usimamizi wa Mungu ni wa ajabu, kwa sababu watu wanafikiri kuwa usimamizi wa Mungu hauna uhusiano wowote na mwanadamu. Wanafikiri kuwa usimamizi wa Mungu ni kazi ya Mungu pekee, shughuli za Mungu, na hivyo wanadamu hawajali kuhusu usimamizi wa Mungu. Kwa njia hii, kuokolewa kwa wanadamu kumekuwa kusiko yakini na kusiko dhahiri, na kumebaki tu maneno matupu. Hata kama mwanadamu anamfuata Mungu ili aokolewe na aingie katika hatima inayopendeza, mwanadamu hajishughulishi na jinsi ambavyo Mungu Hutekeleza kazi Yake. Mwanadamu hashughulishwi na Anachokipanga Mungu na anachopaswa kufanya ili aokolewe.Huzuni iliyoje! Kuokolewa kwa mwanadamu hakuwezi kutenganishwa na usimamizi wa Mungu, aidha hakuwezi kutenganishwa na mipango ya Mungu. Na bado mwanadamu hafikirii chochote kuhusu usimamizi wa Mungu, na hivyo anaendelea kujitenga mbali na Mungu. Kutokana na hayo, idadi ya watu wanaomfuata Mungu inaendelea kuongezeka bila kujua mambo yanayohusiana na kuokolewa kwa mwanadamu kama vile uumbaji ni nini, kuamini kwa Mungu ni nini, jinsi ya kumwabudu Mungu, na kadhalika. Kufikia sasa, basi, lazima tuzungumze kuhusu usimamizi wa Mungu, ndiposa kila mfuasi ajue wazi umuhimu wa kumfuata Mungu na kumwamini. Watakuwa na uwezo wa kuchagua njia watakayoifuata ipasavyo, badala ya kumfuata Mungu tu ili kupata baraka, au kuepukana na majanga, au kuwa na mafanikio.

Alhamisi, 17 Oktoba 2019

Kutanafusi kwa Mwenye Uweza

Kutanafusi kwa Mwenye Uweza

Kutanafusi kwa Mwenye Uweza

Kunayo siri kubwa moyoni mwako, ambayo hujawahi kuifahamu kamwe, kwa sababu umekuwa ukiishi katika ulimwengu bila mwanga. Moyo wako na roho yako vimepokonywa na yule mwovu. Macho yako yamezuiwa kwa giza yasione, na huwezi kuliona jua angani wala nyota ikimetameta wakati wa usiku. Masikio yako yamezibwa na maneno ya udanganyifu, na husikii sauti ya Yehova ingurumayo kama radi, wala sauti ya maji yakitiririka kutoka katika kiti cha enzi. Umepoteza kila kitu ambacho kilipaswa kuwa chako kwa haki, kila kitu ambacho Mwenye uweza alikupa. Umeingia katika bahari ya mateso isiyokuwa na mwisho, bila nguvu ya kukuokoa, bila matumaini ya kurudi ukiwa hai, na yote unayofanya ni kupambana na kusonga kila siku.… Tokea wakati huo, hungeweza kuepuka kuteswa na yule mwovu, uliwekwa mbali na baraka za mwenye Uweza, mbali na kukimu kwa mwenye Uweza, unatembea katika njia ambayo huwezi kurejea nyuma tena. Kuitwa mara milioni hakuwezi kusisimua moyo wako na roho yako. Unalala fofofo mikononi mwa yule mwovu, ambaye amekushawishi katika ulimwengu usio na mipaka, bila mwelekeo na bila alama za barabarani. Tokea hapo, umepoteza hali yako ya asili ya kutokuwa na hatia na utakatifu wako, na kuanza kujificha kutokana na utunzaji wa mwenye Uweza. Ndani ya moyo wako, yule mwovu anakuelekeza katika kila jambo na anakuwa uhai wako. Humwogopi tena, kumwepuka, au kumshuku; badala yake, unamchukulia kama Mungu aliye moyoni mwako. Unaanza kumtunza na kumwabudu, na nyinyi wawili mnakuwa msiotengana kama mwili na kivuli chake, kila akitoa nafsi yake kwa mwingine katika uzima na mauti. Hujui lolote kabisa kuhusu mahali ulikotoka, kwa nini ulizaliwa, au kwa nini utakufa. Unamtazama Mwenye uweza kama mgeni; hujui mwanzo Wake, sembuse yale yote ambayo Amekutendea. Kila kitu kitokacho Kwake kimekuwa cha kuchukiza kwako. Huvitunzi wala kujua thamani yavyo. Unatembea kando na yule mwovu, kuanzia siku ile ulipoanza Mwenye uweza alianza kukukimu. Wewe na yule mwovu mmepitia maelfu ya miaka ya dhoruba na tufani pamoja, na pamoja naye, mnampinga Mungu ambaye alikuwa chanzo cha uhai wako. Hujui lolote kuhusu kutubu, sembuse kwamba umefikia ukingo wa kuangamia. Unasahau kwamba yule mwovu amekujaribu na kukutesa; umesahau asili yako. Kwa njia hii, yule mwovu amekuwa akikuharibu, hatua baada ya hatua, hata mpaka leo. Moyo wako na roho yako vimekufa ganzi na vimeoza. Umeacha kulalamika juu ya maudhi ya dunia ya wanadamu, na huamini tena kwamba dunia si ya haki. Bado hujali sana kama Mwenye uweza yupo. Hii ni kwa sababu ulimchukulia yule mwovu kuwa baba yako wa kweli kitambo, na huwezi tena kutengana naye. Hii ndiyo siri iliyo moyoni mwako.

Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu Ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia

Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu Ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia

Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu Ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia

Je, ungependa kumwona Yesu? Je, ungependa kuishi na Yesu? Je, ungependa kuyasikia maneno yaliyonenwa na Yesu? Iwapo ni hivyo, basi utakaribishaje kurudi kwa Yesu? Je, uko tayari kabisa? Utakaribisha kurudi kwa Yesu kwa namna gani? Nafikiri kuwa kila ndugu anayemfuata Yesu angependa kumpa Yesu makaribisho mazuri. Lakini Je, mmewazia hili: Mtamjua Yesu kweli Atakaporejea? Je, mtaelewa kweli kila kitu Atakachosema? Je, mtakubali kweli, bila masharti, kila kazi ambayo Anafanya? Wale wote ambao wamesoma Biblia wanajua kuhusu kurudi kwa Yesu, na wale wote ambao wamesoma Biblia wanangoja kwa makini kuja Kwake. Nyote mmetazamia kufika kwa wakati huo, na uaminifu wenu ni wa kusifika, imani yenu kweli ni ya kuleta wivu, lakini mnatambua kuwa mmefanya kosa kuu? Yesu Atarejea kwa namna gani? Mnaamini kuwa Yesu Atarudi juu ya wingu jeupe, lakini Nawauliza: Wingu hili jeupe linaashiria nini? Na kwa kuwa wafuasi wengi wa Yesu wanangoja kurejea Kwake, Atashuka miongoni mwa watu wapi? Iwapo ninyi ni wa kwanza kati ya wale ambao Yesu Atawashukia, Je, wengine hawataona jambo hili kama lisilo la haki sana? Najua kuwa nyinyi mna ukweli mkubwa na utiifu kwa Yesu, lakini mmewahi kukutana na Yesu? Mnajua tabia Yake? Mmewahi kuishi na Yeye? Mnaelewa kiasi gani kumhusu kwa kweli? Wengine watasema kuwa maneno haya yanawaweka katika tatizo gumu. Watasema, “Nimesoma Biblia kuanzia mwanzo hadi mwisho mara nyingi sana. Nitakosaje kumwelewa Yesu? Usijali kuhusu tabia ya Yesu—najua hata rangi ya nguo Alizopenda kuvaa. Je, haushushi hadhi yangu ukisema simwelewi?” Napendekeza kuwa usiyapinge masuala haya; ni heri utulie na kufanya ushirika juu ya maswali yafuatayo: Kwanza, unajua uhalisi ni nini, na nadharia ni nini? Pili, unajua dhana ni nini, na ukweli ni nini? Tatu, unajua kile kinachowazwa na kile kilicho halisi?

Jumatano, 16 Oktoba 2019

Jinsi ya Kumjua Mungu Duniani

Nyinyi nyote mna furaha kupokea tuzo mbele ya Mungu na kuwa walengwa wa fadhili Zake machoni Pake. Haya ni matakwa ya kila mtu baada ya yeye kuanza kuwa na imani kwa Mungu, kwani mwanadamu kwa moyo wake wote hujitahidi kupata mambo yaliyo juu na hakuna aliye tayari kubaki nyuma ya wengine. Hii ndiyo njia ya mwanadamu. Kwa sababu hii hasa, wengi kati yenu wanajaribu daima kujipendekeza kwa Mungu mbinguni, lakini kwa kweli, uaminifu wenu na uwazi kwa Mungu ni wa kiasi kidogo sana ukilinganishwa na uaminifu na uwazi wenu kwenu wenyewe. Mbona Nasema hivi? Kwa sababu Sikiri uaminifu wenu kwa Mungu kabisa, na zaidi Nakana kuwepo kwa Mungu aliye ndani ya mioyo yenu. Hiyo ni kusema, Mungu mnayemwabudu, Mungu asiye dhahiri mnayempenda, hayupo kabisa. Kinachonifanya niseme haya kwa uhakika ni kwamba mko mbali sana na Mungu wa kweli. Uaminifu mnaomiliki unatokana na kuwepo kwa sanamu mioyoni mwenu, na kunihusu Mimi, Mungu anayeonekana kama asiye mkubwa wala mdogo machoni penu, mnachofanya ni kunikiri kwa maneno tu. Ninaposema juu ya umbali wenu mkubwa kutoka kwa Mungu, Ninamaanisha jinsi mlivyo mbali sana na Mungu wa kweli, ilhali Mungu asiye dhahiri Anaonekana kuwa karibu. Nisemapo “asiye mkubwa,” inamaanisha jinsi Mungu mnayemwamini siku ya leo anaonekana tu kuwa mwanadamu asiye na uwezo mkubwa; mwanadamu asiye wa fahari sana. Na Nisemapo, “asiye mdogo,” inamaanisha kuwa ingawa mwanadamu huyu hawezi kuita upepo na kuamuru mvua, hata hivyo Anaweza kumwita Roho wa Mungu kufanya kazi inayotingisha mbingu na dunia, hivyo kumchanganya mwanadamu kabisa. Kwa nje, nyote mnaonekana kuwa watiifu sana kwa huyu Kristo aliye duniani, lakini kwa kiini hamna imani Kwake wala kumpenda. Ninachomaanisha ni kwamba yule mliye na imani kwake kwa kweli ni yule Mungu asiye dhahiri katika hisia zenu, na yule kweli mnayempenda ni Mungu mnayemtamani usiku na mchana, lakini bado hamjamwona kamwe kibinafsi. Na kuhusu huyu Kristo, imani yenu ni sehemu tu, na upendo wenu Kwake si kitu. Imani inamaanisha imani na kusadiki; upendo unamaanisha kusujudu na kusifu ndani ya mioyo yenu, bila kuondoka. Lakini imani yenu na upendo wenu kwa Kristo wa siku ya leo vimepunguka chini ya hili. Ikujapo kwa imani, mna imani Kwake jinsi gani? Ikujapo kwa upendo, mnampenda jinsi gani? Hamjui kabisa kuhusu tabia Yake, sembuse kiini Chake, hivyo ni jinsi gani kwamba mna imani Kwake? Uko wapi uhalisi wa imani yenu Kwake? Mnampenda jinsi gani? Uko wapi uhalisi wa upendo wenu Kwake?
Wengi wamenifuata bila kusita hadi leo, na katika miaka hii michache, nyote mmepitia uchovu mwingi. Nimefahamu vizuri tabia ya asili na mazoea ya kila mmoja wenu, na imekuwa vigumu sana kuingiliana nanyi. Cha kusikitisha ni kwamba ingawa nina maarifa nyingi kuwahusu, hamna ufahamu hata kidogo kunihusu. Sio ajabu wengine wanasema mlidanganywa na mwanadamu katika wakati wa mkanganyiko. Hakika, hamwelewi chochote kuhusu tabia Yangu, na hata zaidi hamwezi kufahamu yaliyo akilini Mwangu. Sasa ninyi kunielewa visivyo kunaongezeka haraka, na imani yenu Kwangu inabaki ile imani iliyokanganyika. Badala ya kusema kwamba mna imani na Mimi, ingekuwa bora kusema kwamba nyote mnajaribu kujipendekeza Kwangu na kunibembeleza. Nia zenu ni rahisi sana—yeyote anayeweza kunituza, nitamfuata, na yeyote anayeweza kuniwezesha kutoroka majanga makubwa, nitaamini kwake, awe Mungu ama Mungu fulani yeyote. Hakuna kati ya haya yanayonihusu. Kuna wanadamu wengi kama hao kati yenu, na hali hii ni nzito sana. Ikiwa siku moja, majaribio yatafanywa kuona ni wangapi kati yenu wanamwamini Kristo kwa sababu mna umaizi kuhusu kiini Chake, basi Nahofia kwamba hakuna mmoja wenu atakuwa na uwezo kufanya Ninavyotaka. Hivyo haitakuwa hoja kwa kila mmoja wenu kuzingatia swali hili: Mungu mliye na imani na Yeye ni tofauti sana na Mimi, na kwa hivyo, nini basi ni kiini cha imani yenu kwa Mungu? Kadri mnavyozidi kuamini katika mnayedai kuwa Mungu wenu, ndivyo mnavyozidi kupotea mbali sana nami. Basi, ni nini msingi wa suala hili? Nina uhakika hakuna mmoja wenu amewahi kufikiria suala hili, lakini mmefikiria uzito wake? Mmewaza kuhusu matokeo ya kuendelea na imani ya namna hii?
Sasa, matatizo yaliyowekwa mbele yenu ni mengi, na hakuna mmoja wenu aliye na uhodari wa kuleta ufumbuzi. Iwapo haya yataendelea, basi walio katika hatari ya kupoteza ni nyinyi wenyewe pekee. Nitawasaidia kuyatambua matatizo, lakini itabakia kwenu kupata ufumbuzi.
Nawathamini sana wale wasio na shaka kuhusu wengine na pia nawapenda sana wale wanaokubali ukweli kwa urahisi; kwa aina hizi mbili za wanadamu Ninaonyesha utunzaji mkubwa, kwani machoni Pangu wao ni waaminifu. Kama una udanganyifu mwingi, basi utakuwa na moyo wenye hadhari na mawazo ya shaka juu ya mambo yote na wanadamu wote. Kwa sababu hii, imani yako Kwangu inajengwa kwa msingi wa shaka. Imani kama hii ni moja ambayo kamwe Sitaitambua. Bila imani ya kweli, basi utakuwa mbali hata zaidi na upendo wa kweli. Na ikiwa unaweza kumshuku Mungu na kumkisia utakavyo, basi wewe bila shaka ni mdanganyifu zaidi kati ya wanadamu wengine. Mnakisia iwapo Mungu anaweza kuwa kama mwanadamu: mwenye dhambi isiyosameheka, mwenye tabia ndogondogo, anayependelea na asiye na mantiki, aliyekosa hisia ya haki, mwenye mbinu ovu, mdanganyifu na mjanja, na pia anayefurahishwa na uovu na giza, na kadhalika. Si sababu ambayo mwanadamu ana mawazo kama haya kwamba hana hata ufahamu mdogo wa Mungu? Imani kama hii ni sawa na dhambi! Zaidi ya hayo, kuna hata wale wanaoamini kwamba Sifurahishwi na yeyote isipokuwa wale wanaojirairai na kujipendekeza, na kwamba wale wasio na ujuzi huu hawatakaribishwa na watapoteza nafasi yao katika nyumba ya Mungu. Je, haya ndiyo maarifa ambayo mmepata kwa miaka hii yote mingi? Ni haya ndiyo mliyoyapata? Na ufahamu wenu kunihusu hauko kwa kutoelewa kama huku tu; mbaya hata zaidi ni kukufuru kwenu Roho wa Mungu na kuitukana Mbingu. Hii ndiyo maana Ninasema kwamba imani kama yenu itawasababisha tu kupotea mbali na Mimi na kukuwa na upinzani mkubwa dhidi Yangu. Kwa miaka mingi ya kazi, mmeona ukweli mwingi, lakini mnajua kile masikio Yangu yamesikia? Ni wangapi kati yenu walio tayari kukubali ukweli? Nyote mnaamini kwamba mko tayari kulipa gharama ya ukweli, lakini ni wangapi walioteseka kweli kwa ajili ya ukweli? Yote yaliyo ndani ya mioyo yenu ni uovu, na hivyo mnaamini kwamba yeyote, bila kujali ni nani, ni mjanja na asiye mwaminifu. Hata mnaamini kwamba Mungu mwenye mwili angekuwa bila moyo wa ukarimu na upendo wema kama tu binadamu wa kawaida. Zaidi ya hayo, mnaamini kwamba tabia ya adabu na asili yenye huruma na ukarimu ziko kwa Mungu wa mbinguni pekee. Na mnaamini kwamba mtakatifu kama huyu hayuko, na kwamba giza na uovu tu ndio unaotawala duniani, ilhali Mungu ni kitu ambacho mwanadamu huwekea matumaini yake ya mazuri na mema, na mtu maarufu aliyebuniwa na mwanadamu. Ndani ya akili zenu, Mungu aliye mbinguni ni mnyoofu sana, mwenye haki, na mkubwa, anayestahili ibada na upendezewaji, lakini Mungu huyu aliye duniani ni mbadala tu na chombo cha Mungu aliye mbinguni. Mnaamini Mungu huyu hawezi kuwa sawa na Mungu wa mbinguni, na hata zaidi hawezi kutajwa kwa pumzi moja na Yeye. Ifikapo kwa ukubwa na heshima ya Mungu, ni mali ya utukufu wa Mungu aliye mbinguni, lakini ifikapo kwa tabia na upotovu wa mwanadamu, vinahusishwa na Mungu aliye duniani. Mungu aliye mbinguni daima ni mkuu, ilhali Mungu wa duniani daima ni asiye na maana, mdhaifu na asiyejimudu. Mungu aliye mbinguni haathiriwi na hisia, kwa haki tu, ilhali Mungu aliye duniani ana motisha za kibinafsi tu na Hana haki na mantiki yoyote. Mungu aliye mbinguni hana udanganyifu hata kidogo na daima ni mwaminifu, ilhali Mungu wa duniani daima ana upande mdanganyifu. Mungu aliye mbinguni anampenda sana mwanadamu, ilhali Mungu wa duniani anamjali mwanadamu isivyotosha, hata kumpuuza kabisa. Ufahamu huu usio sahihi umewekwa kwa muda mrefu kwa mioyo yenu na unaweza pia kuendelezwa mbele katika siku za usoni. Mnachukulia matendo yote ya Kristo kwa msimamo wa wadhalimu na kuhukumu kazi Yake yote na utambulisho Wake na kiini Chake kwa mtazamo wa waovu. Mmefanya kosa kubwa sana na kufanya kile ambacho hakijawahi kufanywa na wale kabla yenu. Yaani, mnamtumikia tu Mungu mkuu aliye mbinguni na taji juu ya kichwa Chake na hammshughulikii kamwe Mungu mnayemchukulia kuwa asiye na maana kabisa kiasi cha kutoonekana kwenu. Hii siyo dhambi yenu? Huu sio mfano halisi wa kosa lenu dhidi ya tabia ya Mungu? Mnamwabudu sana Mungu aliye mbinguni. Mnapenda sana sura zilizo kuu na kuheshimu wanaojulikana kwa ajili ya umbuji wao. Mnaamrishwa kwa furaha na Mungu Anayejaza mikono yenu na utajiri, na mnatamani sana Mungu Anayeweza kutimiza tamaa zenu zote. Yule tu msiyemwabudu ni Mungu huyu asiye mkuu; Chombo chenu tu cha chuki ni ushirikiano na huyu Mungu ambaye hakuna mwanadamu anayeweza kumchukulia kuwa mkuu. Kitu pekee ambacho hamko tayari kufanya ni kumtumikia huyu Mungu ambaye hajawahi kuwapa senti hata moja, na Yule tu msiyemtamani ni huyu Mungu asiyependeza. Mungu kama huyu hawezi kuwawezesha kupanua upeo wenu wa macho, kuhisi kana kwamba mmepata hazina, sembuse kutimiza mnachotaka. Mbona, basi, mnamfuata? Je, mmefikiria kuhusu maswali kama haya? Kile ufanyacho hakimkosei huyu Kristo tu; cha muhimu hata zaidi, kinakosea Mungu aliye mbinguni. Nadhani kwamba, haya siyo madhumuni ya imani yenu kwa Mungu!
Mnatamani sana kwa Mungu kufurahishwa nanyi, lakini bado mko mbali sana na Mungu. Tatizo ni nini hapa? Mnakubali tu maneno Yake, lakini sio ushughulikiaji na upogoaji Wake; hata zaidi hamwezi kukubali mpangilio Wake wote, kuwa na imani kamilifu Kwake. Tatizo, basi, ni gani hapa? Kimsingi, imani yenu ni kaka tupu la yai lisiloweza kutoa kifaranga. Kwani imani yenu haijawaletea ukweli ama kuwapa maisha, na badala imewaletea hisia danganyifu ya tumaini na msaada. Madhumuni ya imani yenu kwa Mungu ni kwa ajili ya tumaini hili na msaada huu badala ya ukweli na maisha. Kwa hivyo, Nasema kwamba mkondo wa imani yenu kwa Mungu si mwingine bali ni kujaribu kujipendekeza kwa Mungu kupitia utumwa na kutokuwa na aibu, na hauwezi kuchukuliwa kuwa imani ya kweli hata kidogo. Kifaranga anaweza kujitokezaje kwa imani kama hii? Kwa maneno mengine, ni tunda lipi ambalo imani kama hii inaweza kuzalisha? Azma ya imani yenu kwa Mungu ni kutimiza nia zenu kupitia kumtumia Mungu. Huu sio ukweli zaidi unaoonyesha kosa lenu dhidi ya tabia ya Mungu? Mnaamini kuwepo kwa Mungu aliye mbinguni lakini mnakataa yule Mungu aliye duniani. Hata hivyo, Sikubaliani na maoni yenu. Nawapongeza tu wale wanadamu wanaosimama imara na kumtumikia Mungu wa duniani, kamwe sio wale wasiomkiri Kristo aliye duniani. Bila kujali jinsi wanadamu kama hawa walivyo waaminifu kwa Mungu aliye mbinguni, mwishowe, hawatauepuka mkono Wangu unaoadhibu waovu. Wanadamu kama hawa ni waovu; ni wale waovu wanaompinga Mungu na hawajawahi kumtii Kristo kwa furaha. Bila shaka, idadi yao inajumuisha wale wote wasiomjua na, zaidi, wasiomkiri Kristo. Unaamini kwamba unaweza kutenda utakavyo kwa Kristo alimradi wewe ni mwaminifu kwa Mungu aliye mbinguni? Makosa! Kutomjua Kristo kwako ni kutomjua Mungu aliye mbinguni. Bila kujali uaminifu wako kwa Mungu aliye mbinguni, ni maneno matupu tu na kujifanya, kwani Mungu aliye duniani si muhimu tu kwa mwanadamu kupokea ukweli na ufahamu mkubwa zaidi, lakini hata zaidi ni muhimu kwa lawama ya mwanadamu na baadaye kwa kuushika ukweli kuwaadhibu waovu. Umeelewa matokeo yenye faida na yanayodhuru hapa? Umepata kuyapitia? Ningependa siku moja hivi karibuni ninyi muelewe ukweli huu: Kumjua Mungu, mnapaswa kumjua sio tu Mungu wa mbinguni lakini, hata muhimu zaidi, Mungu aliye duniani. Msiyachanganye yaliyo kipaumbele ama kuruhusu yaliyo ya pili kuchukua nafasi ya yaliyo ya msingi. Ni kwa njia hii tu ndiyo unaweza kujenga uhusiano mzuri na Mungu, kuwa karibu na Mungu, na kupeleka moyo wako karibu na Yeye. Kama umekuwa wa imani kwa miaka nyingi na kushirikiana na Mimi kwa muda mrefu, lakini bado unabaki mbali na Mimi, basi Nasema kwamba ni lazima iwe kuwa mara nyingi unaikosea tabia ya Mungu, na mwisho wako utakuwa mgumu sana kufikiria. Kama miaka mingi ya ushirikiano na Mimi haijakubadilisha kuwa mwanadamu aliye na ubinadamu na ukweli, ila badala yake imeingiza njia zako ovu ndani ya asili yako, na huna maono maradufu ya uwongo kuhusu fahari kuliko awali pekee lakini kutonielewa kwako kumeongezeka pia, kiasi kwamba unakuja kunichukulia kuwa rafiki yako mdogo wa kando, basi Nasema kwamba mateso yako si ya juujuu tena, lakini yamepenya ndani kwa mifupa yako. Yote yaliyosalia ni wewe kusubiri matayarisho ya mazishi yako kufanywa. Huhitaji kunisihi basi Niwe Mungu wako, kwani umetenda dhambi inayostahili kifo, dhambi isiyosameheka. Hata kama Ningeweza kuwa na huruma nawe, Mungu aliye mbinguni Atasisitiza kuchukua maisha yako, kwani kosa lako dhidi ya tabia ya Mungu si shida ya kawaida, lakini lile lililo kubwa sana kiasili. Wakati utakapofika, usinilaumu kwa sababu ya kutokujulisha mbeleni. Yote yanarudia haya: Wakati unashirikiana na Kristo—Mungu aliye duniani—kama mwanadamu wa kawaida, yaani, unapoamini kwamba Mungu huyu si chochote ila ni mwanadamu, ni hapo basi ndipo utaangamia. Hili ndilo onyo Langu la pekee kwenu nyinyi nyote.
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Jumanne, 15 Oktoba 2019

1. Kumjua Mungu ni nini hasa? Kuwa kwa ufahamu wa Biblia na nadharia ya teolojia unaweza kuchukuliwa kama kumjua Mungu?

X. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Jinsi ya Kumjua Mungu

1. Kumjua Mungu ni nini hasa? Kuwa kwa ufahamu wa Biblia na nadharia ya teolojia unaweza kuchukuliwa kama kumjua Mungu?

Maneno Husika ya Mungu:
Kumjua Mungu kunamaanisha nini? Kunamaanisha kwamba mwanadamu anajua shangwe, hasira, huzuni na furaha ya Mungu; huku ndiko kumjua Mungu. Unasema kwamba umemwona Mungu, ilhali huelewi shangwe, hasira, huzuni, na furaha ya Mungu, huelewi tabia Yake, wala huelewi haki Yake. Huna ufahamu wa rehema Zake, na hujui Anachokipenda ama Anachokichukia.Huu si ufahamu wa Mungu. Ikiwa unamjua, unamwelewa, na unaweza kuelewa mapenzi Yake kiasi, basi unaweza kumwamini kwa kweli, kumtii kwa kweli, kumpenda kwa kweli, na kumwabudu Yeye kwa kweli. Ikiwa huelewi mambo haya, basi unafuata tu, mtu fulani anayefuata tu na kufuata umati. Hiyo haiwezi kuitwa kutii kwa kweli au ibada ya kweli. Je! Ibada ya kweli inafanyika vipi? Hakuna wowote wanaomjua Mungu na kumwona Mungu kwa kweli ambao hawamwabudu Yeye, ambao hawamheshimu. Wote lazima wasujudu na kumwabudu Yeye. Kwa sasa, wakati wa kazi ya Mungu mwenye mwili, kadri watu wanavyokuwa na ufahamu zaidi wa asili ya uungu wa Mungu, wa tabia Yake na kile Anacho na alicho, ndivyo wanavyovithamini zaidi na kumcha Yeye. Kwa kawaida, ufahamu mdogo unamaanisha kutokuwa makini zaidi, na kwamba Mungu anachukuliwa kama mwanadamu. Ikiwa watu wanamjua Mungu na kumwona kweli, watatetemeka kwa hofu. Kwa nini Yohana alisema, “Yeye anayekuja baada ya mimi ni mwenye nguvu kuniliko, ambaye mimi si wa kufaa kubeba viatu vyake”? Ijapokuwa ufahamu wa ndani ya moyo wake haukuwa wa kina kirefu sana, lakini alijua kwamba Mungu ni wa ajabu. Ni watu wangapi wanaoweza kumcha Mungu sasa? Bila kuijua tabia Yake, mtu anawezaje kumheshimu? Ikiwa watu hawajui kiini cha Kristo na hawaelewi tabia ya Mungu, hawawezi kumwabudu Mungu wa vitendo kwa kweli. Ikiwa watu wanaona tu kuonekana kwa nje kwa kawaida kwa Kristo na hawajui asili Yake, ni rahisi kwa wao kumchukulia Kristo kama mtu wa kawaida. Huenda wakachukua mtazamo usio wa heshima Kwake, wanaweza kumdanganya, kumkataa, kutomtii, na kutoa hukumu Kwake. Wanaweza kujiona kuwa sahihi na kuchukulia neno Lake na kazi Yake kama yasiyo na maana, wahodhi mawazo kumhusu Mungu, na kumshutumu na kumkufuru. Ili kutatua masuala haya mtu lazima ajue kiini cha Kristo, uungu wa Kristo. Hiki ndicho kipengele kikuu cha kumjua Mungu; ni kile waumini wote wanapaswa kutimiza.

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

Kunayo mambo mengi ambayo Ninatumai mtaweza kufikia. Hata hivyo, matendo yenu na maisha yenu yote hayawezi kutimiza kwa ujumla mahitaji Yangu, kwa hiyo lazima Nilenge suala moja kwa moja na kuwafafanulia moyo na akili Zangu. Tukichukulia kwamba uwezo wenu wa utambuzi na ufahamu wenu vyote ni duni sana, karibu mmekosa kabisa kujua tabia na dutu Yangu, na hivyo ni suala la dharura kwangu Mimi kuwafahamisha kuhusu haya. Haijalishi hapo awali ulielewa kiwango kipi au kama uko radhi kuelewa masuala haya, lazima bado Niyaelezee kwenu kwa undani.

Jumatatu, 14 Oktoba 2019

Neno la Mwenyezi Mungu|Maonyo Matatu

Kazi ya Mungu,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu

Neno la Mwenyezi Mungu|Maonyo Matatu

Kama muumini wa Mungu, hamfai kuwa watiifu kwa yeyote mwingine isipokuwa Yeye katika mambo yote na mjilinganishe na moyo Wake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa wote huelewa mafundisho haya, ukweli huu wa kimsingi ulio wazi kabisa kwa binadamu hauwezi kuonekana kuwa kujumuishwa kwao kikamilifu, kutokana na ugumu wao, kama vile hali yao ya kutojua, upuzi, au ufisadi. Kwa hivyo, kabla mwisho wenu haujaamuliwa, Ninafaa kuwaambia kwanza baadhi ya mambo, ambayo ni yenye umuhimu mkubwa sana kwenu.

Jumapili, 13 Oktoba 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Wewe U Mwaminifu kwa Nani?

kazi ya Mungu,Sauti ya Mungu,kumjua Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Wewe U Mwaminifu kwa Nani?

Kila siku mnayoiishi sasa ni ya maana sana na muhimu sana kwa hatima yenu na majaliwa yenu, kwa hivyo mnapaswa kufurahia kila mlicho nacho na kila dakika inayopita. Mnapaswa kutumia muda wenu vizuri ili muweze kujinufaisha, ili msije kuishi maisha haya bure. Pengine mnajihisi kukanganyikiwa mnaojiuliza ni kwa nini Ninazungumza maneno haya. Kwa kweli, Sijapendezwa na matendo ya yeyote kati yenu. Kwa maana matumaini ambayo Nimekuwa nayo juu yenu si vile tu mlivyo sasa. Kwa hivyo, Naweza kuelezea hivi: Nyinyi nyote mko hatarini kabisa. Vilio vyenu vya kwanza kwa ajili ya wokovu na matamanio yako ya kwanza ya kufuatilia ukweli na kutafuta nuru vinakaribia mwisho.

Jumamosi, 12 Oktoba 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako

Kazi ya Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako

Nimefanya kazi nyingi miongoni mwenu na, ni wazi kwamba, Nimezungumza vizuri pia. Hata hivyo, Nahisi kwamba maneno na kazi Yangu havijatimiza lengo la kazi Yangu ya siku za mwisho. Maana, katika siku za mwisho, kazi Yangu si kwa ajili ya mtu au watu fulani bali ni kwa manufaa ya kufafanua tabia Yangu asilia. Hata hivyo, kutokana na sababu nyingi—pengine ukosefu wa muda au shughuli nyingi za kazi—tabia Yangu haijamwezesha binadamu kunijua hata kidogo.

Ijumaa, 11 Oktoba 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Kazi ya Mungu,neno la Mungu,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Njia ya maisha si kitu ambacho kinaweza kumilikiwa na mtu yeyote tu, wala hakipatikani kwa urahisi na wote. Hiyo ni kwa sababu maisha yanaweza kuja tu kutoka kwa Mungu, ambayo ni kusema, Mungu Mwenyewe tu ndiye Anamiliki mali ya maisha, hakuna njia ya maisha bila Mungu Mwenyewe, na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote.

Alhamisi, 10 Oktoba 2019

Neno la Mwenyezi Mungu|Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu



Neno la Mwenyezi Mungu|Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu

Enzi ya zama ishaenda, na enzi mpya imefika. Mwaka baada ya mwaka na siku baada ya siku, Mungu amefanya kazi nyingi. Alikuja duniani, kisha Akaondoka. Mzunguko kama huu umeendelea kwa vizazi vingi. Siku ya leo, Mungu anaendelea kama mbeleni kufanya kazi Anayopaswa kufanya, kazi ambayo bado Hajaikamilisha, kwani hadi leo, bado Hajaingia mapumzikoni. Kutoka wakati wa uumbaji hadi leo, Mungu amefanya kazi nyingi, lakini ulijua kwamba kazi anayoifanya Mungu leo ni nyingi kuliko awali na kipimo ni kikubwa zaidi? Hii ndiyo maana Nasema Mungu amefanya jambo kubwa miongoni mwa wanadamu.

Jumatano, 9 Oktoba 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli

Kazi ya siku za mwisho ni kutenganisha vitu vyote kulingana na jinsi yavyo, kuhitimisha mpango wa usimamizi wa Mungu, kwa maana muda u karibu na siku ya Mungu imewadia. Mungu huwaleta wote ambao wameingia katika ufalme Wake, yaani, wale wote ambao wamekuwa waaminifu Kwake mpaka mwisho, katika enzi ya Mungu Mwenyewe. Hata hivyo, kabla ya kuja kwa enzi ya Mungu Mwenyewe, kazi Atakayofanya Mungu si kutazama matendo ya mwanadamu wala kuchunguza maisha ya wanadamu, ila ni kuhukumu uasi wake, kwa maana Mungu atawatakasa wale wote wanaokuja mbele ya kiti Chake cha enzi.

Jumatatu, 7 Oktoba 2019

Neno la Mwenyezi Mungu|Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?

Kazi ya Mungu,Neno la Mungu,Mwenyezi Mungu

Neno la Mwenyezi Mungu|Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?

Huenda ikawa safari yako ya imani katika Mungu imekuwa ndefu zaidi ya mwaka mmoja au miwili, na labda kwa maisha yako umestahimili ugumu mwingi miaka hii yote; au labda haujapitia ugumu na badala yake umepokea neema nyingi. Kuna uwezekano pia kuwa hujapitia ugumu wala kupokea neema, na badala yake umeishi maisha ya kawaida tu. Hiyo haijalishi, kwani wewe bado u mfuasi wa Mungu, kwa hivyo tushikiriane kuhusu mada ya kumfuata Mungu. Lakini, lazima Niwakumbushe wote wanaoyasoma maneno haya kwamba neno la Mungu huelekezwa kwa wale wanaomtambua na wale wanaomfuata Mungu, na sio kwa watu wote wa ulimwengu, wakiwemo wale wasiomtambua Mungu.

Jumapili, 6 Oktoba 2019

Neno la Mwenyezi Mungu | Unapaswa Kutafuta Njia ya Uwiano na Kristo


Neno la Mwenyezi Mungu | Unapaswa Kutafuta Njia ya Uwiano na Kristo

Nimefanya kazi kubwa miongoni mwa binadamu, na maneno ambayo Nimeeleza wakati huu yamekuwa mengi. Maneno haya ni kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu, na yalikuwa yanaeleza ili binadamu aweze kulingana na Mimi. Ilhali Nimewapokea watu wachache tu duniani ambao wanalingana na Mimi, na hivyo Nimesema kwamba binadamu hathamini maneno Yangu, kwa kuwa binadamu halingani na Mimi. Kwa njia hii, kazi ambayo Naifanya sio tu kwa ajili ya mwanadamu aweze kuniabudu; muhimu zaidi, ni kwa ajili ya mwanadamu aweze kulingana na Mimi.

Jumamosi, 5 Oktoba 2019

Neno la Mwenyezi Mungu | Wengi Wameitwa, Lakini Wachache Wamechaguliwa

Kazi ya Mungu,Sauti ya Mungu,Umeme wa Mashariki

Neno la Mwenyezi Mungu | Wengi Wameitwa, Lakini Wachache Wamechaguliwa

    Nimewatafuta wengi duniani wawe wafuasi Wangu. Kati yao ni wale wanaohudumu kama makuhani, wanaoongoza, wanaojumuisha wana, wanaojumuisha watu, na wale wanaotoa huduma. Ninawagawa katika makundi haya tofauti kwa msingi wa uaminifu wanaonionyesha. Wakati wanadamu wote wameainishwa kulingana na aina, yaani, asili ya kila aina ya mwanadamu inapowekwa wazi, basi Nitamhesabu kila mwanadamu miongoni mwa aina yake kamili na kuweka kila aina katika nafasi yake kamili ili Nikamilishe lengo Langu la ukombozi wa mwanadamu.

Ijumaa, 4 Oktoba 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu


Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu

Watu wote wana tamaa ya kuona uso wa kweli wa Yesu na wote hutaka kuwa pamoja Naye. Naamini kuwa hakuna mmoja wa ndugu au dada anayeweza kusema kwamba yeye hana nia ya kumwona au kuwa pamoja na Yesu. Kabla ya nyinyi kumwona Yesu, yaani, kabla ya nyinyi kumwona Mungu Aliye kwenye mwili, mnaweza kuwa na mawazo mengi, kwa mfano, kuhusu sura ya Yesu, njia Yake ya kuzungumza, njia Yake ya maisha, na kadhalika. Hata hivyo, wakati mmemwona hasa, mawazo yenu yatabadilika haraka. Ni kwa nini? Je, mnataka kujua? Hata ingawa fikira za mwanadamu hakika haziwezi kupuuzwa, haikubaliki hata zaidi kwa mwanadamu kubadilisha kiini cha Kristo.

Alhamisi, 3 Oktoba 2019

Matamshi ya Kristo | Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu Ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Je, ungependa kumwona Yesu? Je, ungependa kuishi na Yesu? Je, ungependa kuyasikia maneno yaliyonenwa na Yesu? Iwapo ni hivyo, basi utakaribishaje kurudi kwa Yesu? Je, uko tayari kabisa? Utakaribisha kurudi kwa Yesu kwa namna gani? Nafikiri kuwa kila ndugu anayemfuata Yesu angependa kumpa Yesu makaribisho mazuri. Lakini Je, mmewaza iwapo mtamjua Yesu kweli Atakaporejea? Je, mtaelewa kweli kila kitu Atakachosema? Je, mtakubali kweli, bila masharti, kila kazi ambayo Anafanya? Wale wote ambao wamesoma Biblia wanajua kuhusu kurudi kwa Yesu, na wale wote ambao wamesoma Biblia wanangoja kwa makini kuja Kwake. 

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu (Sehemu ya Pili)

kazi ya Mungu,Neno la Mungu,ukweli

Matamshi ya Mwenyezi Mungu|Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu (Sehemu ya Pili)

Punde tu Shetani anaposhindwa, hivyo ni kusema, punde tu mwanadamu anaposhindwa kabisa, mwanadamu ataelewa kwamba kazi yake yote ni kwa ajili ya wokovu, na kuwa mbinu ya wokovu huu ni kurejesha kutoka kwa mikono ya Shetani. Miaka 6,000 ya kazi ya Mungu ya usimamizi imegawanywa katika awamu tatu: Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Awamu hizi zote tatu za kazi ni kwa ajili ya wokovu wa wanadamu, ambayo ni kusema, ni kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu ambaye ameharibiwa na Shetani kwa kiasi kikubwa. Wakati huo huo, hata hivyo, pia ni ili kwamba Mungu afanye vita na Shetani.