Smiley face

Alhamisi, 30 Novemba 2017

Sura ya 28. Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu



Kutoa kwenu "muhtasari kuhusu ukweli" hakufanywi ili kuwawezesha watu kupata maisha au kupata mabadiliko katika tabia zao kutoka kwa ukweli. Badala yake, kunafanywa ili watu waweze kuwa weledi wa maarifa na mafundisho fulani kutoka kwa ukweli. Wao huonekana kana kwamba wanaelewa lengo lililokusudiwa katika kazi ya Mungu, wakati kwa kweli wamekuwa weledi wa baadhi ya maneno ya mafundisho tu. Hawaelewi maana iliyokusudiwa ya ukweli, na si tofauti na kusomea theolojia au kusoma Biblia. 

Sura ya 23. Jinsi ya kuelewa Umoja wa Mwili na Roho


Baadhi ya watu huuliza, “Mungu huangalia kwa makini moyo wa binadamu, na mwili na Roho wa Mungu ni moja. Mungu hujua kila kitu ambacho watu husema, kwa hivyo Mungu anajua kwamba sasa ninamwamini?” Kujibu hili swali huhusisha jinsi ya kuelewa Mungu mwenye mwili na uhusiano kati ya Roho Wake na mwili. Baadhi husema, “Mungu ni halisi kwa njia thabiti.” Wengine husema, “Yeye ni halisi kwa njia thabiti. 

Jumatano, 29 Novemba 2017

Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo | Ufahamu wa Kuokolewa


Lin Qing Jijini Qingzhou, Mkoa wa Shandong
Kwa miaka hii mingi ya kumfuata Mungu, nimeacha furaha ya familia yangu na mwili, na nimekuwa na shughuli nyingi siku nzima nikitimiza wajibu wangu kanisani. Kwa hiyo niliamini: Mradi tu nisiache kazi katika kanisa ambayo nimeaminiwa, nisimsaliti Mungu, nisiache kanisa, na kumfuata Mungu hadi mwisho, nitahurumiwa na kuokolewa na Mungu. Niliamini pia kuwa nilikuwa nikitembea katika njia ya wokovu na Mungu, na yote niliyokuwa niyafanye ni kumfuata Yeye mpaka mwisho.

Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo | Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka


Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka


Baixue Mji wa Shenyang
Kwa sababu ya mahitaji ya kazi, nilihamishiwa hadi sehemu nyingine ya kazi. Wakati huo, nilikuwa na shukurani sana kwa Mungu. Nilihisi kwamba nilikuwa ninapungukiwa sana, lakini kwa njia ya ukuzwaji mtakatifu na Mungu, nilipewa nafasi ya kutimiza wajibu wangu katika eneo la kazi la ajabu hivyo. Niliweka nadhiri kwa Mungu moyoni mwangu: Ningefanya lote ninaloweza kumlipa Mungu. Hata hivyo, baada ya kufika, nilitambua utata mwingi katika kazi iliyokuwa ikifanyika. Matokeo yake, nilichukua jukumu mwenyewe la kuanza kukagua kila kitu cha kazi.

Jumanne, 28 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Nane )



13. Bwana Yesu Ala Mkate na Kuonyesha Maandiko Baada ya Kufufuka Kwake
Luka 24:30-32 Na ikatimia, alipokuwa akikaa na wao ili wale, aliuchukua mkate, na kuubariki, na akaupasua, na kuwapa. Na macho yao yakafunguka, na wakamjua, na akatoweka wasimwone. Na wakaambiana, je, Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu sisi, wakati alipokuwa akituzungumzia njiani, na wakati alipotufungulia maandiko?

Sura ya 39. Tofauti Kati Ya Mabadiliko Ya Nje Na Mabadiliko Katika Tabia



Ni nini mnafahamu kuhusu mabadiliko katika tabia? Asili ya mabadiliko katika tabia na mabadiliko katika mwenendo ni tofauti, na mabadiliko katika matendo pia ni tofauti—yote ni tofauti kwa asili. Watu wengi wanaweka mkazo maalum kwa tabia yao katika imani yao kwa Mungu, matokeo yakiwa mabadiliko yanayofanyika katika mienendo yao. Baada ya kuamini katika Mungu, wanakoma kubishana na wengine, wanakoma kupigana na watu na kuwatukana, wanakoma kuvuta sigara na kunywa, hawaibi mali ya uma—hata iwe msumari ama kipande cha mbao pekee—na hata wanaenda kiasi cha kutoipeleka kotini wanapopata hasara ama wamekosewa. 

Jumatatu, 27 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Saba )



Sasa hebu tusome dondoo za maandiko zilizo hapa chini.
12. Maneno ya Yesu kwa Wanafunzi Wake Baada ya Kufufuka Kwake
(Yohana 20:26-29) Na baada ya siku nane wanafunzi wake walikuwa ndani tena, na Tomaso pamoja nao: Kisha akaja Yesu, na milango imefungwa, na akasimama katikati, kisha akasema, Amani iwe kwenu. Kisha akamwambia Tomaso, Weka hapa kidole chako, na utazame mikono yangu; na ulete mkono wako uuweke ubavuni mwangu, na usiwe asiyeamini, bali uwe aaminiye. Naye Tomaso akajibu akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! Yesu akamwambia, Tomaso, kwa kuwa umeniona, umeamini; heri wanayo wale ambao hawajaona, ilhali wameamini.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Sita )



10. Hukumu ya Wafarisayo kwa Yesu.
(Marko 3:21-22) Na rafiki zake waliposikia kulihusu, wakatoka kwenda kumkamata: kwa maana walisema, Amerukwa na akili. Na waandishi walioshuka kutoka Yerusalemu wakasema, Ana Beelzebuli, na kwa mwana wa kifalme wa pepo huwatoa pepo.

Jumapili, 26 Novemba 2017

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa, Umeme wa Mashariki,
Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa
I
Nilitaka kulia lakini hakuna mahali palihisi sawa. Nilitaka kuimba lakini hakuna wimbo ulipatikana. Nilitaka kuonyesha upendo wa kiumbe aliyeumbwa. Nikitafuta juu na chini, lakini hakuna maneno yangeweza kusema, yangeweza kusema jinsi hasa ninavyohisi. Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Nainua mikono yangu kwa sifa, ninafurahia kwamba Ulikuja katika dunia hii.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Tano )



Halafu, hebu tuangalie vifungu vifuatavyo katika maandiko.
9. Bwana Yesu Atenda Miujiza
1) Bwana Yesu Awalisha Watu Elfu Tano
Yohana 6:8-13 Mmoja wa wanafunzi wake, Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akasema kwake, Kuna mvulana hapa, aliye na mikate mitano ya shayiri nao samaki wawili wadogo: lakini ni yapi miongoni mwa watu wengi? Naye Yesu akasema, Wafanye watu waketi chini. Na kulikuwa na nyasi nyingi pahali hapo. Kwa hivyo wanaume wakaketi chini, wakiwa idadi ya takribani elfu tano.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Nne )



Halafu hebu tusome fahamu zifuatazo.
6. Ibada Mlimani
Sifa na Heri (Mat 5:3-12)
Chumvi na Nuru (Mat 5:13-16)
Sheria (Mat 5:17-20)

Jumamosi, 25 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Tatu )


Kifuatacho tutaangalia mfano uliozungumziwa na Bwana Yesu katika Enzi ya Neema.
3. Mfano wa Kondoo Aliyepotea
Mat 18:12-14 Mnafikiri vipi? Iwapo mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao apotee, je, hawaachi hao tisini na tisa, na kuenda milimani, na amtafute huyo ambaye amepotea? Na iwapo atampata, kweli nawaambia, anafurahi zaidi kwa sababu ya huyo kondoo, kuliko wao tisini na tisa ambao hawakupotea. Kwa namna hiyo siyo mapenzi ya Baba yenu ambaye yuko mbinguni, kuwa mmoja wa hawa wadogo aangamie.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III(Sehemu ya Pili )


Mwenyezi Mungu alisema: Tumezungumza tu kuhusu kazi yote ambayo Mungu amekamilisha, misururu ya mambo Aliyoyafanya kwa mara ya kwanza. Kila mojawapo ya mambo haya yanahusiana na mpango wa Mungu wa usimamizi na mapenzi ya Mungu. Yanahusiana pia na tabia binafsi ya Mungu na kiini Chake. Kama tunataka kuelewa bora zaidi kile Alicho nacho Mungu na kile Alicho, hatuwezi kukoma katika Agano la Kale au katika Enzi ya Sheria, lakini tunahitaji kusonga mbele pamoja na hatua ambazo Mungu alichukua katika kazi Yake. Hivyo basi, Mungu alipotamatisha Enzi ya Sheria na kuanza Enzi ya Neema, hatua zetu binafsi zimefika katika Enzi ya Neema—enzi iliyojaa neema na ukombozi.

Ijumaa, 24 Novemba 2017

Sura ya 34. Umuhimu na Mazoezi ya Sala



Mwenyezi Mungu alisema: Je, mnaomba vipi kwa sasa? Ni maendeleo kwa sala za kidini jinsi gani? Mnaelewa nini hasa kuhusu umuhimu wa sala? Je mmechunguza maswali haya? Kila mtu ambaye hafanyi sala ako mbali na Mungu, kila mtu ambaye hasali anafuata mapenzi yake; Kukosekana kwa sala kunaashiria kwenda mbali na Mungu na usaliti wa Mungu. Ni nini uzoefu wenu hasa na sala? Sasa hivi, kazi ya Mungu tayari inakaribia mwisho na uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu unaweza kuonekana kutoka kwa maombi ya mwanadamu.

Sura ya 33. Jinsi ya Kufahamu Tabia Yenye Haki ya Mungu



Watu wanaweza kupangwa kwa makundi, ambayo hubainishwa kwa roho zao. Watu wengine wana roho za binadamu, na wao huchaguliwa kwa njia iliyoamuliwa kabla. Ndani ya roho ya binadamu kuna sehemu iliyoamuliwa kabla. Watu wengine hawana roho; wao ni pepo ambao wamepenyeza. Hawajaamuliwa kabla na kuchaguliwa na Mungu. Ingawa wamekuja ndani, hawawezi kuokolewa, na hatimaye wataondolewa na pepo. Inaamuliwa na asili ya ndani ya mtu huyo iwapo ataikubali kazi ya Mungu, au njia ipi atakayochukua au iwapo ataweza kubadilika baada ya kuikubali.

Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo | Kiini cha Ulipizaji Kisasi wa Mtu Binafsi



Kiini cha Ulipizaji Kisasi wa Mtu Binafsi


Zhou Li Mji wa Xintai, Mkoa wa Shandong
Wakati fulani kitambo, tulihitaji kuzichora wilaya katika eneo letu, na kwa msingi wa kanuni zetu kwa ajili ya uteuzi wa viongozi, kulikuwa na ndugu mmoja wa kiume aliyekuwa mtaradhia mzuri kiasi. Nilitayarisha kumpandisha cheo hadi kuwa kiongozi wa wilaya. Siku moja nilipokuwa nikizungumza na ndugu huyu, alitaja kwamba alihisi kuwa nilikuwa mwenye nguvu sana katika kazi yangu, mkali sana, na kwamba katika mkusanyiko pamoja nami hapakuwa na furaha nyingi ....

Alhamisi, 23 Novemba 2017

Ishini Katika Upendo wa Mungu | Dansi ya Sifa "Wimbo wa Mapenzi Matamu"

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa, Umeme wa Mashariki,

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa, Umeme wa Mashariki,
Wimbo wa Mapenzi Matamu
Kinani mwa moyo wangu, ni mapenzi Yako. Ni matamu sana, nakaa karibu yako. Kukutunza hukoleza moyo wangu; kukutumikia na mawazo yangu yote. Kuongoza moyo wangu, ni mapenzi Yako; mimi hufuata nyayo zako za mapenzi. Mimi hujisogeza kulingana na macho Yako; mapenzi yanaonyesha furaha ya moyo wangu. Mapenzi yanaonyesha furaha ya moyo wangu. Sasa mimi huishi katika ulimwengu mwingine, hakuna yeyote isipokuwa wewe uko nami. Unanipenda, ninakupenda; hakuna huzuni wala sikitiko hutusumbua. Hakuna huzuni wala sikitiko hutusumbua. Kumbukumbu chungu hutokomea. Kumbukumbu chungu hutokomea.

Sura ya 31. Jinsi ya Kufahamu Uenyezi na Utendaji wa Mungu



Mwenyezi Mungu alisema: Kitu hiki kinachoitwa mwanadamu kina uwezo wa kumsaliti Mungu, kwa hivyo unaweza kujua nini kutoka kwa hili? Baadhi ya watu huuliza: "Mungu alimuumba mwanadamu kwa hivyo Mungu hawezi kumzuia mwanadamu kumsaliti Yeye? Ni kwa nini mwanadamu bado ana uwezo wa kumsaliti Mungu? Je, Mungu si mwenyezi?" Hili ni tatizo, sio? Ni tatizo gani unaloweza kuona hapa katika suala hili? Mungu ana upande wa vitendo, lakini pia Ana upande wa uenyezi.

Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo | Kutambua Kuwa Nimekuwa Nikiitembea Njia ya Mafarisayo


Kutambua Kuwa Nimekuwa Nikiitembea Njia ya Mafarisayo


Wuxin Mji wa Taiyuan, Mkoa wa Shanxi
Kitu ambacho tumezungumzia mara kwa mara katika ushirikiano wa awali ni njia ambazo zilitembewa na Petro na Paulo. Inasemekana kwamba Petro alizingatia kujijua mwenyewe na kumjua Mungu, na alikuwa mtu ambaye Mungu alimpenda, ilhali Paulo alizingatia tu kazi yake, sifa na hadhi yake, na alikuwa mtu ambaye Mungu alimdharau. Daima nimekuwa na hofu ya kuitembea njia ya Paulo, ambayo ndiyo sababu mimi kwa kawaida mara nyingi husoma maneno ya Mungu kuhusu uzoefu wa Petro ili kuona jinsi alivyopata kumjua Mungu.

Jumatano, 22 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II(Sehemu ya Saba )


Msiwe na Wasiwasi Wowote Kuhusu Majaribio ya Mungu


Mwenyezi Mungu alisema, Baada ya kuupokea ushuhuda kutoka kwa Ayubu kufuatia mwisho wa majaribio yake, Mungu aliamua kwamba angepata kundi au zaidi ya kundi—la watu kama Ayubu, ilhali aliamua kutowahi tena kumruhusu Shetani kushambulia au kunyanyasa mtu yeyote mwingine kwa kutumia mbinu ambazo alikuwa amemjaribu, akamshambulia na kumnyanyasa Ayubu, kwa kucheza karata na Mungu; Mungu hakumruhusu Shetani tena kufanya mambo kama hayo kwa binadamu ambaye ni mnyonge, mjinga, na asiyejua—ilikuwa tosha kwamba Shetani alikuwa amemjaribu Ayubu! Kutomruhusu Shetani kuwanyanyasa watu vyovyote anavyotaka ndiyo rehema ya Mungu. 

Upendo wa Mungu Huushinda Moyo wa Mwanadamu | " Wimbo wa Kifuasi cha Dhati " Video Rasmi ya Muziki

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa, Umeme wa Mashariki,
Wimbo wa Kifuasi cha Dhati

Wimbo wa Kifuasi cha Dhati


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa, Umeme wa Mashariki,
Wimbo wa Kifuasi cha Dhat
Kuna Mmoja hapa, Yeye ni Mungu katika mwili.  Anayoyasema, Anayoyafanya, yote ni ukweli.Hekima Yake, Uadilifu Wake, nayapenda yote. Kukutana Naye, kumpata Yeye, nimebarikiwa sana. Kuna Mmoja hapa, Yeye ni Mungu katika mwili. Anayoyasema, Anayoyafanya, yote ni ukweli. Hekima Yake, uadilifu Wake, nayapenda yote. Kukutana Naye, kumpata Yeye, nimebarikiwa sana. Moyo wake, Upendo wake, vimefanya nishindwe. Mpe upendo, mfuate Yeye, ah mpendwa wangu. Nampenda, najihisi mtamu, teseka kwa ajili Yake. Mpate, ishi kwa ajili Yake, mpende milele.

Jumanne, 21 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II (Sehemu ya Sita )


Ushuhuda wa Ayubu Waleta Tulizo kwa Mungu

Mwenyezi Mungu alisema: Nikikwambia sasa kwamba Ayubu ni mtu mzuri, huenda usiweze kutambua maana yaliyomo kwenye maneno haya, na huenda usiweze kung’amua mawazo yaliyopo katika yale maneno Niliyoyaongea kwa ujumla; lakini subiri mpaka siku ile utakapokuwa umepitia majaribio sawa na au yale yanayofanana na yale ambayo Ayubu alipitia, wakati utakapokuwaumepitia magumu, wakati utakapokuwa umepitia majaribio wewe binafsi yaliyopangiliwa kwa ajili yako na Mungu, wakati utakapojitolea kila kitu ulichonacho, na kuvumilia udhalilishaji na ugumu, ili kuweza kushinda Shetani na kuwa na ushuhuda kwa Mungu katikati ya majaribio hayo yote—basi utaweza kutambua maana ya maneno haya Ninayoyaongea.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II(Sehemu ya Tano)


Kuhusu Ayubu

Mwenyezi Mungu alisema: Baada ya kusikia namna Ayubu alivyopitia majaribio, kunao uwezekano kwamba wengi wenu watataka kujua maelezo zaidi kuhusu Ayubu mwenyewe, hasa kuhusiana na siri iliyomfanya akapata sifa za Mungu. Hivyo basi leo, hebu tuzungumzie kuhusu Ayubu!

Toeni Nyimbo za Sifa kwa Mungu | Muziki wa Akapela " Mpende Mungu Wa Vitendo Kwa Moyo Wetu Wote "

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Kanisa, Umeme wa Mashariki,
Mpende Mungu Wa Vitendo Kwa Moyo Wetu Wote

La … la la la … la la la…. 
La … la la la … la la la … la…. Jua la haki lapanda kutoka Mashariki. Ee Mungu! Utukufu wako hujaza mbingu na dunia. Mpenzi mrembo, upendo Wako huzingira moyo wangu. Watu wanaofuatilia ukweli wote wanampenda Mungu. Ingawa mimi huamka peke yangu asubuhi mapema, Ninahisi furaha ninapotafakaria neno la Mungu. Maneno mororo ni kama mama mpenzi, maneno ya hukumu kama baba mkali. (Ala….) Sipendi chochote duniani; kwa moyo wangu wote ninampenda Mungu wangu tu.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II(Sehemu ya Nne)


Kutotikisika kwa Uadilifu wa Ayubu Kunaleta Aibu Kwake Shetani na Kusababisha Shetani Kutoroka kwa Wasiwasi


Mwenyezi Mungu alisema: Na ni nini ambacho Mungu alifanya wakati Ayubu alipopitia mateso haya? Mungu aliangalia, na kutazama, na Akasubiri matokeo. Wakati Mungu Alipokuwa akiangalia na kutazama, Alihisi vipi? Alihisi kuwa mwenye huzuni, bila shaka. Lakini, kutokana na huzuni Yake, Aliweza kujuta ruhusa Yake kwa Shetani ya kumjaribu Ayubu? Jibu ni, La, Asingefanya hivyo. Kwani Yeye alisadiki kwa dhati kwamba Ayubu alikuwa mtimilifu na mnyofu, kwamba alimcha Mungu na kujiepusha na maovu. Mungu alikuwa amempa Shetani tu fursa ya kuthibitisha uhaki wa Ayubu mbele ya Mungu, na kufichua maovu yake Shetani na hali ya kudharauliwa kwake binafsi.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II(Sehemu ya Tatu)



Mwenyezi Mungu alisema: Kuanzia mwanzo hadi leo, ni binadamu tu ambaye ameweza kuzungumza na Mungu. Yaani, miongoni mwa viumbe wote walio hai na viumbe wa Mungu, hakuna yeyote isipokuwa binadamu ameweza kuzungumza na Mungu. Binadamu anayo masikio yanayomwezesha kusikia, na macho yanayomwezesha kuona, anayo lugha na fikira zake binafsi, na pia anao uhuru wa kuamua chochote. 

Jumatatu, 20 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II(Sehemu ya Pili)



Kwenye kipindi sawa na kile cha Ibrahimu, Mungu pia aliliangamiza jiji. Jiji hili liliitwa Sodoma. Bila shaka, watu wengi wanaijua hadithi ya Sodoma, lakini hakuna yeyote aliyejua fikira za Mungu zilikuwa usuli wa kuangamiza Kwake jiji hili.
Na hivyo leo, kupitia mazungumzo yake Mungu na Ibrahimu hapa chini, tutajifunza fikira Zake wakati huo, huku pia tukijifunza kuhusu tabia Yake. Kinachofuata, hebu tusome vifungu vya maandiko.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I (Sehemu ya Nne)



3. Mungu Atumia upinde wa mvua kuasisi agano na mwanadamu.
(Mwa 9:11-13) Na Nitalithibitisha agano langu nanyi, wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika; wala hakutakuwa tena gharika kuiharibu nchi. Na Mungu akasema, Hii ndiyo ishara ya agano Ninalofanya kati yangu na nyinyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote mpaka milele: Mimi Nauweka upinde wangu mawinguni, na utakuwa ni ishara ya agano kati yangu na nchi. Kisha, hebu tuangalie sehemu hii ya maandiko kuhusu namna Mungu alivyounda upinde wa mvua kama ishara ya Agano lake na binadamu.

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I(Sehemu ya Pili)



Mwenyezi Mungu alisema: Ili kuelewa tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe lazima muanzie na jambo dogo sana. Jambo hilo dogo sana mnalopaswa kuanzia ni nini? Kwanza kabisa, Nimezikusanya baadhi ya sura kutoka kwenye Biblia. Taarifa iliyo hapa chini inayo mistari ya Biblia, ambayo yote inahusiana na mada ya tabia ya Mungu, kazi ya Mungu na Mungu Mwenyewe. Nilipata dondoo hizi mahususi kama nyenzo za marejeleo ili kuwasaidia kujua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. 

Jumapili, 19 Novemba 2017

Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake(Sehemu ya Pili)


Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Uepuke na Maovu

Mwenyezi Mungu alisema: Kunao msemo ambao unafaa kutilia maanani. Ninasadiki msemo huu ni muhimu sana, kwa sababu kwangu Mimi unakuja akilini mara nyingi kila siku. Kwa nini hivyo? Kwa sababu kila wakati Ninapokumbana na mtu, kila wakati Ninaposikia hadithi ya mtu, kila wakati Ninaposikia kile alichopitia mtu au ushuhuda wake wa kusadiki Mungu, siku zote Ninatumia msemo huu kuweza kupima kama mtu huyu binafsi ni mtu wa aina ambayo Mungu anataka au la, mtu wa aina ambayo Mungu anapenda. 

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I(Sehemu ya Tatu)


Mwenyezi Mungu alisema: Kisha, tutazungumzia hadithi ya Nuhu na namna ambavyo inahusiana na mada ya kazi ya Mungu, tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe.
Mnaona Mungu akimfanya nini Nuhu kwenye sehemu hii ya maandiko? Pengine kila mmoja aliyeketi hapa anajua kitu kuhusu hayo baada ya kusoma maandiko: Mungu alimfanya Nuhu kujenga safina, kisha Mungu akatumia gharika kuangamiza ulimwengu. 

Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake(Sehemu ya Tatu)


Namna Ambavyo Mungu Huanzisha Matokeo Ya Binadamu na Kiwango Ambacho Huasisi Matokeo ya Binadamu

Mwenyezi Mungu alisema: Kabla ya kuwa na mitazamo au hitimisho zenu binafsi, mnafaa kwanza kuelewa mwelekeo wa Mungu kwenu, kile ambacho Mungu anafikiria, na kuamua kama kufikiria kwako ni sahihi au la. Mungu hajawahi kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya mtu, na Hajawahi kutumia kiwango cha mateso yaliyovumiliwa na mtu katika kuasisi matokeo yake. Basi Mungu hutumia kiwango gani katika kuasisi matokeo ya binadamu? Kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya binadamu—hii ndiyo inaingiliana zaidi na dhana za watu.

Jumamosi, 18 Novemba 2017

Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake(Sehemu ya Nne)

<

Elewa Mwelekeo wa Mungu na Utupilie Mbali Dhana zote Potoshi Kumhusu Mungu

 

Mwenyezi Mungu alisema: Mungu huyu ambaye kwa sasa unasadiki umewahi kufikiria kuhusu Yeye kuwa ni Mungu wa aina gani? Anapomwona mtu mwovu akifanya mambo maovu, je Anayachukia? (Anayachukia.) Anapoona makosa ya mtu asiyejua, mwelekeo Wake ni upi? (Huzuni.) Anapowaona watu wakiiba sadaka Yake, mwelekeo Wake ni upi? (Anawachukia.) Haya yote yako wazi, sivyo? Anapoona mtu akiwa mzembe katika kusadiki Mungu, na mtu huyo akikosa kutafuta ukweli kwa namna yoyote, mwelekeo wa Mungu ni upi? Bado hujaelewa jambo hili, sivyo? Uzembe ni mwelekeo ambao si dhambi, na humkosei Mungu.

Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake(Sehemu ya Tano)


Hatima ya Binadamu Inaamuliwa na Mwelekeo Wake Kwa Mungu


Mwenyezi Mungu alisema: Mungu ni Mungu aliye hai, na kama vile tu watu wanavyotenda tofauti katika hali tofauti, ndivyo mwelekeo wa Mungu ulivyo katika utendakazi huu na unavyotofautiana kwa sababu Yeye si kikaragosi, wala Yeye si hewa tupu. Kupata kuujua mwelekeo wa Mungu ni jambo lenye thamani kwa wanadamu. Watu wanafaa kujifunza vipi, kwa kuujua mwelekeo wa Mungu, wanaweza kuijua tabia ya Mungu na kuuelewa moyo Wake kidogo kidogo. Mnapouelewa moyo wa Mungu kidogo kidogo hamtahisi kwamba kumcha Mungu na kujiepusha na maovu ni jambo gumu la kutimiza.

Sura ya 30. Kumtumikia Mungu Mtu Anapaswa Kutembea Njia ya Petro



Watu wengi hawawezi kuainisha ni watu gani wana ukweli, watu gani hawana ukweli na watu gani husema mambo yaliyo na ukweli. Unapoulizwa kueleza ni nini maana ya "ukweli," huwezi kueleza kwa wazi. Lakini mara tu mtu anaposema kitu, unasema: “Mtazamo wake ni wa kweli. Maneno ayasemayo yanaonyesha ufahamu wa utendaji uliopatikana kupitia kwa uzoefu.” Unaelewa mara tu unapowasikia wakizungumza. Kwa ninyi hapa mlio wapya, Nikiwauliza ni nini maana ya 'uhalisi,' hamtaweza tu kunijibu, lakini pia hamtaweza kueleza tofauti kati ya mtu anayezungumza uhalisi na mtu anayezungumza mafundisho ya dini.

Ijumaa, 17 Novemba 2017

Sura ya 29. Mtu Lazima Ajue Jinsi Ambayo Mungu Hufanya Kazi


Mwenyezi Mungu alisema: Kazi ya Mungu, iwe ni kwa mwili au kwa Roho, yote inafanywa kulingana na mpango wa usimamizi. Kazi Yake haifanywi kulingana na kama ni ya umma au ya kibinafsi, au kulingana na mahitaji ya mwanadamu—inafanywa kikamilifu kulingana na mpango wa usimamizi. Hatua hii ya kazi haiwezi kufanywa kwa njia yoyote ya zamani: Inapaswa kukamilika juu ya msingi wa hatua mbili zilizopita za kazi. Hatua ya pili ya kazi iliyokamilishwa wakati wa Enzi ya Neema ilimpa mwanadamu ukombozi. Hii ilifanywa na Mungu mwenye mwili.

Sura ya 27. Ni Nini Maana ya “Kumkosea Mungu”


Ukilibadilisha au kulikanganya neno la Mungu Mwenyewe, basi hiyo ni sawa na uasi wa Mungu, kukufuru dhidi Yake na usaliti. Hii ni sawa tu na malaika mkuu kusema:"Mungu, Unaweza kuumba mbingu na ardhi na vitu vyote na Unaweza kufanya miujiza, lakini pia mimi ninaweza. Unapanda juu kwenye kiti cha enzi, na hivyo hivyo mimi pia napanda. Unatawala mataifa yote, Ninatawala mataifa yote pia. Wewe ulimuumba mwanadamu ilhali mimi ninawatawala!" Je, hii si ya hali sawa? Wengine wana mtazamo fidhuli kuhusu mipangilio ya kazi kutoka juu. 

Sura ya 21. Ukimbizaji Ukweli Tu Ndiyo Imani ya Kweli katika Mungu



Kama huna uzoefu wa kitu, basi wewe hakika hutajua jinsi ya kukisimamia na utakisimamia vibaya. Hata kama unakisimamia, na ufikiri: “Mimi nimeeleza kiasi haya yote na nikasema mengi kulihusu. Wao pia wamelisikiza mara nyingi. Nimeongea sana kulihusu. Nafikiri yote ambayo nimeshiriki kuhusu tatizo hili kimsingi ni kweli, sivyo?” lakini kwa kweli, yote tu ni mafundisho, na wewe unatumia mafundisho kutatua tatizo. Mbona unasema ni mafundisho? 

Alhamisi, 16 Novemba 2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini na Nne

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,
Tamko la Ishirini na Nne

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini na Nne


Mwenyezi Mungu alisema: Kuadibu kwangu kunawajia watu wote, lakini pia kunakaa mbali na watu wote. Maisha yote ya kila mtu yamejaa upendo na pia chuki Kwangu, na hakuna mtu ambaye amewahi kunijua na kwa hivyo mtazamo wa mwanadamu Kwangu ni wa sitasita, na hauna uwezo wa kuwa kawaida. Lakini Nimekuwa Nikimlea na kumchunga mwanadamu na ni kwa sababu ya upumbavu wake ndiyo maana hana uwezo wa kuona matendo Yangu yote na kuelewa nia Zangu. Mimi Ndiye Ninayeongoza katika mataifa yote, na ndiye Mkubwa Zaidi kwa watu wote; kwa ufupi ni kwamba mwanadamu hanijui Mimi. 

Sura ya 19. Maana ya Mungu Kuupitia Uchungu wa Dunia



Mungu anapata mwili ili ateseke kwa niaba ya mwanadamu, na kwa kufanya hivyo atasababisha hatima iliyo ya ajabu ambayo itafuata kwa ajili ya mwanadamu. Hatua hiyo ya kazi iliyokamilishwa na Yesu ilikuwa tu kuwa Kwake mfano wa mwili wenye dhambi na kusulubiwa, kuhudumu Kwake kama sadaka ya dhambi na kuwakomboa wanadamu wote, na hii iliweka msingi wa kuingia kwa baadaye kwa mwanadamu katika hatima iliyo ya ajabu. 

Sura ya 17. Ufahamu wa Kupata Mwili



Kumjua Mungu kunapaswa kufanywa kupitia kwa kusoma neno la Mungu na kulielewa neno la Mungu. Watu wengine husema: "Sijamwona Mungu mwenye mwili, hivyo nitawezaje kumjua Mungu?" Neno la Mungu kwa kweli ni maonyesho ya tabia ya Mungu. Kutoka kwa neno la Mungu unaweza kuuona upendo wa Mungu kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na jinsi Anavyowaokoa ... kwa sababu neno la Mungu linaonyeshwa na Mungu ikilinganishwa na Mungu kumtumia mwanadamu kuliandika. Linaonyeshwa na Mungu binafsi. 

Jumatano, 15 Novemba 2017

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu(Sehemu ya Kwanza )


Tabia ya Haki ya Mungu

Mwenyezi Mungu alisema: Kwa vile sasa mumesikiliza kikao cha ushirika uliopita kuhusu mamlaka ya Mungu, Ninao ujasiri kwamba mumejihami vilivyo na mseto wa maneno kuhusu suala hili. Kiwango unachoweza kukubali, kushika, na kuelewa vyote hivi vinategemea na jitihada zipi utakazotumia. Ni tumaini Langu kwamba utaweza kutazamia suala hili kwa dhati; kwa vyovyote vile hufai kulishughulikia shingo-upande! Sasa, je, kujua mamlaka ya Mungu ni sawa na kujua Mungu kwa uzima wake? 

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)(Sehemu ya Kwanza )


Mamlaka ya Mungu (I)

Vikao vyangu mbalimbali vya ushirika vilivyopita vilikuwa vinahusu kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. Baada ya kuvisikiliza vikao hivi vya ushirika, je, unahisi kuwa umefaidi na kupata ufahamu na maarifa kuhusu tabia ya Mungu? Ufahamu wako na maarifa ni mkubwa kiwango gani? Je, unaweza kuweka nambari katika kiwango hicho? Je, vikao hivi vya ushirika vilikupa ufahamu wa kina kuhusu Mungu? Inaweza kusemwa ufahamu huu ni maarifa ya kweli ya Mungu? 

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Kumi na Tatu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,
Tamko la Kumi na Tatu


Mwenyezi Mungu alisema: Dhamira Zangu kadhaa zimefichwa ndani ya matamshi ya sauti Yangu. Ila mwanadamu hajui na hafahamu chochote kuhusu haya, huku akiendelea kuyapokea na kuyafuata maneno Yangu kutoka nje bila kung’amua roho Yangu na kuelewa mapenzi Yangu kutoka ndani ya maneno Yangu. Ijapokuwa nimeyaweka maneno Yangu wazi, kuna aliyefahamu? Nilitoka Sayuni Nikaja miongoni mwa wanadamu. 

Jumanne, 14 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II(Sehemu ya Kwanza )



Mwenyezi Mungu alisema: Kwenye mkutano wetu wa mwisho tuliweza kuzungumzia mada muhimu sana. Je, wakumbuka mada hiyo ilikuwa kuhusu nini? Hebu Niirudie. Mada ya ushirika wetu wa mwisho ilikuwa: Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. Je, mada hii ni muhimu kwako? Ni sehemu gani katika mada hii ni muhimu kwako? Kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, au Mungu Mwenyewe? Ni sehemu ipi inakuvutia zaidi? Ni sehemu ipi unayotaka kusikiliza kuhusu zaidi? 

Sura ya 16. Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo


Mwenyezi Mungu alisema, Ndani ya familia ya Mungu, kuna imani kadhaa tofauti katika Mungu; imani hizi tofauti lazima zitambulishwe ili kuona wewe ni wa gani.Na imani ya aina ya kwanza, ambayo pia ni aina bora zaidi, mtu huyo ana uwezo wa kuyaamini maneno ya Mungu katika vitu vyote; ana uwezo wa kukubali ufichuzi wote wa Mungu, ushugulikiaji, na upogoaji; yeye ni mwagalifu kwa mapenzi ya Mungu, hupenda, ni mwaminifu kwa, na humwabudu Mungu, na ako tayari kutenda ukweli. 

Sura ya 15. Kutoka katika Siasa Isiyo na Kadri hadi Kutafuta kuwa Msaliaji



1. Uhamaji wa Watu kuelekea kwenye Siasa Isiyo na Kadri
Mwenyezi Mungu alisema: Je, nyote mmekuwa mkitafuta nini hivi karibuni? Je, imekuwa mabadiliko ya tabia na kuwa na ushuhuda wa Mungu? Haijakuwa hiyo! Nawaona watu wengi tena wakitafuta kufa kwa ajili ya Mungu ili kumuaibisha Shetani. Je, mnasubiri tu kuadhibiwa badala ya kupanga kutenda ukweli ama kutafuta kubadilishwa kwa tabia, kulipiza upendo wa Mungu? Baada ya kusoma “Usaliti (1) “na “Usaliti (2), “watu walikuwa na mipango ya kufa. 

Jumatatu, 13 Novemba 2017

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III


Mwenyezi Mungu alisema: Vikao hivi kadhaa vya ushirika vimekuwa na athari kubwa kwa kila mmoja wa watu. Kwa sasa, watu wanaweza hatimaye kuhisi uwepo wa kweli wa Mungu na kwamba Mungu kwa hakika yuko karibu sana na wao. Ingawa watu wamemwani Mungu kwa miaka mingi, hawajawahi kuelewa kwa kweli mawazo na fikira Zake kama wanavyozielewa sasa, wala hawajawahi kupata kwa kweli uzoefu wa matendo Yake halisi kama walio nao kwa sasa.

Sura ya 13. Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao



1. Hakuna Ambaye Angeokolewa iwapo Mungu Angeangalia Tu Maonyesho ya Asili ya Watu
Mwenyezi Mungu alisema: Kwa sasa, utendaji wa watu unaamua matokeo yao, lakini huu utendaji ni upi? Je, unaujua? Nyinyi mnaweza kufikiri kwamba hili linarejelea tabia ya watu iliyopotoka ikijionyesha kazini mwao, lakini halimaanishi lile. Utendaji huu unanena kuhusu ikiwa unaweza kuweka ukweli kwenye vitendo au la na ikiwa unaweza kusalia mwaminifu na kujizatiti unapotenda wajibu wako au la, na vilevile mtazamo wako wa kumwamini Mungu, msimamo wako kwa Mungu, uamuzi wako wa kuteseka kwa ajili ya ugumu, mtazamo wako kwa kukubali hukumu na kupogolewa, kiwango chako cha mabadiliko na idadi ya dhambi kubwa. 

Sura ya 12. Mapenzi ya Mungu ni Kuwaokoa Watu kwa Kiwango Kikubwa Sana Kinachowezekana



1. Usijishughulishe na Ikiwa Umejaaliwa na Mungu, bali Ujishughulishe na Ufuatiliaji Wako
Mwenyezi Mungu alisema: Watu wengi hawaelewi mapenzi ya Mungu; wanafikiri kuwa kila mtu ambaye ameamuliwa na Mungu ataokolewa bila kuepuka na wanafikiri kuwa kila mtu asiyeamuliwa na Mungu hataokolewa hata wakiyafanya mambo vyema zaidi. Wanafikiri kwamba Mungu hataamua matokeo ya watu kulingana na utendaji na tabia yao. Iwapo unafikiri hivi, basi unamwelewa Mungu visivyo kabisa. 

Jumapili, 12 Novemba 2017

Sura ya 11. Kutatua Asili na Kutenda Ukweli


1. Uhusiano Kati ya Ubinadamu na Uwezo wa Kutenda Ukweli
Mwenyezi Mungu alisema: Watu husema kuwa kutenda ukweli ni vigumu kabisa. Basi mbona watu wengine wanaweza kutenda ukweli? Watu wengine husema ni kwa sababu kwa asili wanaipokea kazi ya Roho Mtakatifu ikifanya kazi juu yao, na pia kwa sababu ni wazuri kiasili. Hoja hii ina kiwango fulani cha mantiki. Watu wengine ni wazuri kiasili; wana uwezo wa kutenda ukweli. 

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I(Sehemu ya Kwanza )



Mwenyezi Mungu alisema: Leo tunawasiliana kuhusu mada muhimu. Hii ni mada ambayo imezungumziwa tangu kuanza kwa kazi ya Mungu mpaka sasa, na inayo umuhimu mkuu kwa kila mtu. Kwa maneno mengine, hili ni suala ambalo kila mmoja atakutana nalo kwenye mchakato wote wa kusadiki kwake katika Mungu na suala ambalo lazima lizungumziwe. Ni suala muhimu, lisiloepukika ambalo mwanadamu hawezi kujitenganisha nalo. 

Jumamosi, 11 Novemba 2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini na Moja

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,
Kanisa la Mwenyezi Mungu  Tamko la Ishirini na Moja

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini na Moja


Mwenyezi Mungu alisema: Mwanadamu huanguka katikati ya mwanga Wangu, na anasimama imara kwa sababu ya wokovu Wangu. Niletapo wokovu ulimwenguni kote, mwanadamu hujaribu kutafuta njia za kuingia miongoni mwa mtiririko wa marejesho Yangu, ilhali kuna watu wengi ambao huoshwa wasijulukane waliko na gharika hii ya urejesho; kuna watu wengi ambao wamezama na kumezwa na mafuriko haya na kuna watu wengi pia ambao husimama imara huku kukiwa na mafuriko, ambao hawajawahi kupoteza hisia zao za mwelekeo, na ambao wamefuata mafuriko mpaka sasa. 

Sura ya 10. Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata



1. Kama hali ya Watu Ni Ya Kawaida Inategemea na Kama Wanapenda Ukweli au La
Mwenyezi Mungu alisema: Watu wengi wameibua suala lifuatalo: Baada ya ushirika wa juu, wanahisi wazi kabisa, wanakuwa na nguvu zaidi, na hawana hisia hasi—lakini hali kama hiyo inabaki tu kwa karibu siku kumi, ambapo baadaye hawawezi kudumisha hali ya kawaida. Suala ni nini? Je mmewahi kujiuliza kinachosababisha hili? Mbona hali zenu ni nzuri sana katika siku hizo takriban kumi za kwanza? Wengine wanasema kuwa hili ni tokeo la kutolenga ukweli. 

Kanisa la Mwenyezi Mungu|Tamko la Kumi Na Sita

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,
Kanisa la Mwenyezi Mungu|Tamko La Kumi Na Sita

Kanisa la Mwenyezi Mungu|Tamko La Kumi Na Sita

Mwenyezi Mungu alisema: Kuna mengi Mimi natamani kumwambia mwanadamu, mambo mengi sana ambayo lazima Nimwambie. Lakini uwezo wa mwanadamu wa kukubali una upungufu mwingi: Hana uwezo wa kuyaelewa kabisa maneno Yangu kulingana na kile Ninachokitoa, na anaelewa kipengele kimoja tu lakini haelewi vingine. Lakini Simmalizi mwanadamu kwa ajili ya ukosefu wa nguvu wake, wala Siudhiki na udhaifu wake. 

Ijumaa, 10 Novemba 2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,
Kanisa la Mwenyezi Mungu  Tamko la Ishirini

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini


Mwenyezi Mungu alisema: Utajiri wa jumba Langu ni bila idadi na usioeleweka, lakini mwanadamu hajawahi kuja Kwangu kuufurahia. Hana uwezo wa kuufurahia mwenyewe, wala wa kujilinda mwenyewe kwa kutumia juhudi zake mwenyewe; badala yake, yeye daima huweka imani yake kwa wengine. Kati ya wale wote Ninaowatazamia, hakuna mtu aliyewahi kunitafuta kwa makusudi na moja kwa moja. Wao wote huja mbele Zangu kwa kushawishiwa na wengine, wakiwafuata watu wengi, na hawana nia ya kulipa gharama au kutumia muda kustawisha maisha yao.